Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 22:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Malaika wa Yawe akamwita Abrahamu mara ya pili kutoka mbinguni,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 22:15
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Zaidi ya hayo, malaika wa Yawe akamwambia Hagari: “Nitawazidisha wazao wako hata wasiweze kuhesabika kwa wingi wao.”


Malaika wa Yawe akamukuta Hagari kwenye chemichemi ya maji katika jangwa, chemichemi iliyokuwa katika njia kuelekea Suri.


Mumoja wao akasema: “Hakika nitakurudilia kwa wakati kama huu katika mwaka na muke wako Sara atakuwa na mutoto mwanaume.” Sara alikuwa kule nyuma kwenye mulango wa hema, akisikiliza.


Kwa hiyo, Abrahamu akapaita pahali pale: “Yawe anajalia,” kama inavyosemwa hata leo: “Kwa mulima wa Yawe, watu wanajaliwa.”


akamwambia: “Yawe anasema hivi: Nimeapa kwa nafsi yangu mwenyewe kwamba kwa sababu umefanya hivi, wala haukuninyima mwana wako wa pekee,


Malaika wa Mungu akaongea nami katika ndoto hiyo, akaniita: ‘Yakobo’, nami nikaitika, ‘Niko hapa!’


na malaika ambaye aliniokoa katika mabaya yote, awabariki vijana hawa! Jina langu na majina ya babu zangu, Abrahamu na Isaka, yadumishwe katika vijana hawa; nao waongezeke kwa wingi katika dunia.”


Basi, malaika wa Yawe akamutokea katika mwali wa moto katikati ya kichaka. Musa akaangalia, akashangaa kuona kichaka kinawaka moto na wala hakiungui.


Mimi nimeapa kwa nafsi yangu, ninachosema ni ukweli, neno langu halitarudi nyuma: kila mwanadamu atanipigia magoti, kila mutu atafanya kiapo.


basi, hapo nami nitakumbuka agano langu na Abrahamu, Isaka na Yakobo na kukumbuka ile inchi niliyowaahidia.


Siku hiyo, mimi Yawe nitawalinda wakaaji wa Yerusalema. Wanaokuwa wazaifu zaidi kati yao watakuwa na nguvu kama mufalme Daudi. Wazao wa Daudi watashika usukani kwa kuwaongoza watu wa Yuda kama Mungu, au kama malaika wa Yawe.


Malaika wa Yawe akamwonya Kuhani Mukubwa Yoshua, akamwambia:


“Kulipopita miaka makumi ine, malaika wa Bwana akamutokea Musa katikati ya kichaka kilichokuwa kikiwaka moto katika jangwa karibu na mulima Sinai.


Wakati Mungu alipomupa Abrahamu ahadi, alifanya vilevile kiapo. Kwa sababu hakuna mutu mwingine mukubwa kuliko yeye kusudi ataje jina lake, akaapa kwa jina lake mwenyewe.


Halafu yule malaika niliyemwona akisimama juu ya bahari na inchi kavu akainua mukono wake wa kuume juu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ