Halafu Abrahamu akainua macho, akaona kondoo dume, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi, akakwenda, akamutwaa yule kondoo, akamutoa sadaka ya kuteketezwa kwa moto pahali pa mwana wake.
Halafu Yakobo akamwambia: “Tafazali, ninakuomba uniambie jina lako.” Lakini yeye akamwambia: “Kwa nini kuniuliza jina langu?” Kisha akamubariki Yakobo.
Enyi watu wa Sayuni, mulie na kugaagaa kama mwanamuke anayezaa! Maana sasa mutaondoka katika muji huu muende kukaa katika mbuga, mutakwenda mpaka Babeli. Lakini kule, mutaokolewa. Kule Yawe atawakomboa toka katika makucha ya waadui zenu.
Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.