Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 22:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Lakini malaika wa Yawe akamwita kutoka mbinguni: “Abrahamu! Abrahamu!” Naye akaitika: “Niko hapa!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 22:11
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Malaika wa Yawe akamukuta Hagari kwenye chemichemi ya maji katika jangwa, chemichemi iliyokuwa katika njia kuelekea Suri.


Mungu akamusikia mutoto yule akilia, na malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni, akamwambia: “Una shida gani Hagari? Usiogope. Mungu amesikia sauti ya mutoto kule anapokuwa.


Simama umwinue mutoto na kumushika vizuri katika mikono yako, maana nitamufanya akuwe baba wa taifa kubwa.”


Nyuma ya mambo yale, Mungu alimupima Abrahamu. Mungu alimwita: “Abrahamu!” Naye akaitika: “Niko hapa.”


Abrahamu akanyoosha mukono wake, akatwaa kisu tayari kumuchinja mwana wake.


Malaika akamwambia: “Usinyooshe mukono wako juu ya kijana wala usimufanyie jambo lolote! Sasa ninajua kwamba unamwogopa Mungu, maana haukuninyima hata mwana wako wa pekee.”


akamwambia: “Yawe anasema hivi: Nimeapa kwa nafsi yangu mwenyewe kwamba kwa sababu umefanya hivi, wala haukuninyima mwana wako wa pekee,


Yawe, Mungu wa mbingu, aliyenitoa katika nyumba ya baba yangu na kutoka katika inchi nilimozaliwa, na ambaye alisema nami, aliniapia kwamba atawapa wazao wangu inchi hii. Yeye atamutuma malaika wake mbele yako kusudi umuletee mwana wangu muke kutoka kule.


Malaika wa Mungu akaongea nami katika ndoto hiyo, akaniita: ‘Yakobo’, nami nikaitika, ‘Niko hapa!’


Basi, Israeli akamwambia Yosefu: “Unajua wandugu zako wanachunga nyama kule Sekemu. Kwa hiyo ninataka kukutuma kwao.” Yosefu akajibu: “Niko tayari.”


Mungu akaongea na Israeli katika maono usiku, akamwita: “Yakobo! Yakobo!” Yakobo akaitika: “Niko hapa.”


na malaika ambaye aliniokoa katika mabaya yote, awabariki vijana hawa! Jina langu na majina ya babu zangu, Abrahamu na Isaka, yadumishwe katika vijana hawa; nao waongezeke kwa wingi katika dunia.”


Basi, malaika wa Yawe akamutokea katika mwali wa moto katikati ya kichaka. Musa akaangalia, akashangaa kuona kichaka kinawaka moto na wala hakiungui.


Yawe alipoona kwamba Musa amegeuka kwa kuangalia kichaka, akamwita pale kutoka kichaka: “Musa! Musa!” Musa akaitika: “Niko hapa. Ninasikiliza!”


Kisha nikamusikia Yawe akisema: Nimutume nani? Ni nani atakayekuwa mujumbe wetu? Nami nikajibu: Niko hapa! Unitume mimi.


Sisi wote tukaanguka chini, na nikasikia sauti iliyoniambia hivi katika luga ya Kiebrania: ‘Saulo, Saulo, kwa sababu gani unanitesa? Unajiumiza bure kama ngombe anayepiga teke kwenye chongo ya fimbo ya mwenyeji wake.’


Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo, sababu gani unanitesa?”


Malaika wa Yawe aliondoka Gilgali, akaenda Bokimu, akawaambia Waisraeli: “Niliwaondoa katika inchi ya Misri na kuwaleta katika inchi ambayo niliahidi kwa kiapo kwa babu zenu. Nilisema kwamba sitalivunja agano langu nanyi hata kidogo.


Kisha Yawe akakuja na kusimama hapo, akamwita Samweli kama pale mbele: “Samweli! Samweli!” Samweli akasema: “Sema, maana mimi mutumishi wako ninasikiliza.”


Halafu Yawe akamwita Samweli, naye Samweli, akaitika: “Niko hapa!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ