Mutu mumoja aliyeponyoka, akakwenda kumwarifu Abramu Mwebrania ambaye alikuwa anaishi karibu na mielo ya Mamure Mwamori. Mamure alikuwa ndugu ya Eskoli na Aneri. Wote walikuwa wamefanya agano na Abramu.
Wakati mufalme wa Misri alipowaachilia Waisraeli wajiendee, Mungu hakuwapitisha katika inchi ya Wafilistini, ingawa njia hiyo ilikuwa ya karibu. Mungu alisema: “Sipendi watu hawa wabadilishe nia na kurudi Misri wakijua kama itawapasa kupigana vita.”