Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 21:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Naye akakwenda kando, akaikaa umbali wa kama metre mia moja hivi, akisema ndani ya moyo wake: “Heri nisimwone mwana wangu akikufa.” Na alipokuwa amekaa pale, mutoto akalia kwa sauti kubwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 21:16
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati maji yalipomwishia katika lile chupa, Hagari akamulalisha mwana wake chini ya muti.


Esau akamwambia baba yake: “Baba, maana yake una baraka moja tu? Unibariki hata mimi, ee baba!” Halafu Esau akalia kwa sauti kubwa.


Kisha Yakobo akamubusu Rakeli na kulia kwa sauti.


Nitaweza namna gani kumurudilia baba yangu bila kijana huyu? Siwezi kuvumilia kuona hasara itakayomupata baba yangu.”


Huyo mwanamuke akamwambia: “Kama vile Yawe Mungu wako anavyoishi, sina mukate hata kidogo. Niko tu na unga unaoweza kujaa mukono mumoja katika chungu na mafuta kidogo katika chupa. Nimefika hapa kuokota kuni, kisha niende kwangu kupika chakula hicho, mwana wangu na mimi tukule, kisha tungojee kufa.”


Yule mwanamuke aliyekuwa mama ya huyo mutoto anayekuwa muzima alishikwa na huruma juu ya mwana wake, akamwambia mufalme: “Tafazali mufalme, musimwue mutoto. Mumupe mwenzangu huyo mutoto mwenye kuwa muzima, amutwae yeye.” Lakini yule mwanamuke mwingine akasema: “Hapana! Mutoto asikuwe wangu wala wake. Mumukate vipande viwili.”


Maana, ninaweza namna gani kuvumilia kuona watu wangu wanaangamizwa na wandugu zangu wanauawa?”


Lakini Yawe anasema: Munafikiri kwamba mama anaweza kumusahau mutoto anayemunyonyesha, wala kumuchukia mutoto wa tumbo lake? Hata kama mama anaweza kumusahau mutoto wake, mimi sitakusahau hata kidogo.


Yawe anasema: Muvae magunia, enyi watu wangu na kugaagaa katika majivu. Muomboleze kwa uchungu, kama mutu anayemulilia mwana wake wa pekee, maana mwangamizaji atakuja, na kuwashambulia kwa rafla.


Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa kilio, na nyimbo zenu za furaha kuwa maombolezo. Nitawavalisha ninyi wote magunia kwa huzuni na kunyoa vichwa vyenu upaa, kama kuomboleza kifo cha mutoto wa pekee. Na siku ya mwisho itakuwa ya uchungu mukubwa.


Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.


Kisha akafunga safari yake na kurudia kwa baba yake. “Alipokuwa angali mbali kidogo, baba yake akamwona, akamusikilia huruma. Akamukimbilia, akamukumbatia mwana wake na kumubusu.


Malaika wa Yawe alipowaambia watu wote wa Israeli maneno haya, wakalalamika na kulia.


Yawe awajalie, kila mumoja wenu apate mume na nyumba yake.” Kisha Naomi akawaaga kwa kuwabusu. Lakini wao walianza kulia kwa sauti


Basi, Yawe akuwe mwamuzi kati yangu na wewe. Yeye aliangalie jambo hili, anitetee na kuniokoa katika mikono yako.”


Halafu Daudi na watu wake wakaanza kulalamika, wakalia mpaka walipoishiwa nguvu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ