Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 21:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Hivyo, asubui mapema, Abrahamu akatwaa chakula na chupa la maji, akamupa Hagari na kumubebesha mutoto juu ya bega. Akamufukuza pamoja na mwana wake. Hagari akaondoka, akakuwa anatangatanga katika jangwa la Beri-Seba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 21:14
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Malaika wa Yawe akamukuta Hagari kwenye chemichemi ya maji katika jangwa, chemichemi iliyokuwa katika njia kuelekea Suri.


Asubui mapema, Abrahamu alikwenda pahali alipokuwa akisimama mbele ya Yawe.


Na juu ya huyo mwana wa mujakazi wako nitamufanya akuwe baba wa taifa kubwa kwa sababu yeye vilevile ni mutoto wako.”


Wakati maji yalipomwishia katika lile chupa, Hagari akamulalisha mwana wake chini ya muti.


Kwa hiyo kisima hicho kikaitwa Beri-Seba, maana wote wawili walifanya kiapo pahali pale.


Abrahamu akapanda muti wa mukwaju kule Beri-Seba, akaomba kwa jina la Yawe, akamwabudu Mungu, Mungu wa milele.


Basi, Abrahamu akawarudilia wale watumishi wake, nao pamoja wakaondoka, wakarudi Beri-Seba. Abrahamu akakaa kule Beri-Seba.


Basi, kesho yake, Abrahamu akaamuka asubui mapema, akatandika punda wake, akawatwaa watumishi wake wawili pamoja na Isaka mwana wake. Akatayarisha kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto, kisha akaanza safari kuelekea pahali alipoambiwa na Mungu.


Mutumishi wa Abrahamu na watu aliokuja nao wakakula, wakakunywa na kulala kule. Walipoamuka asubui, mutumishi yule akasema: “Ninaomba kurudi kwa bwana wangu.”


Lakini akawapa wana wa habara zake zawadi. Na wakati alipokuwa bado muzima, akawapeleka katika inchi ya upande wa mashariki, mbali na mwana wake Isaka.


Kesho yake wakaamuka asubui mapema na kufanya kiapo. Kisha Isaka akawasindikiza na kuagana nao kwa amani.


Basi, Isaka akakiita kisima hicho Siba, ni kusema “Kiapo”. Kwa hiyo jina la muji ule ni Beri-Seba hata leo.


Yakobo akaamuka asubui mapema, akatwaa lile jiwe alilokuwa ameliweka chini ya kichwa chake, akalisimika kama nguzo na kulitakasa kwa kulimiminia mafuta.


mutu mumoja akamukuta akitangatanga katika mbuga, akamwuliza: “Unatafuta nini?”


Basi, Israeli akaanza safari yake pamoja na mali yake yote. Alipofika Beri-Seba, akatoa sadaka kwa Mungu wa baba yake Isaka.


Elia akakimbilia katika muji wa Beri-Seba katika jimbo la Yuda, kule alikomwacha mutumishi wake,


Bila kupoteza wakati, mufalme Hezekia akawakusanya wakubwa wa muji, akaenda nao katika nyumba ya Yawe.


Wamoja walitangatanga katika jangwa tupu, hawakuweza kufikia katika muji wa kukaa.


Bila kukawia ninafanya haraka kushika amri zako.


Anayemusalimia jirani yake kwa kelele asubui mapema, itahesabiwa kwamba amemutakia laana.


Mutu aliyepotea mbali na kwake ni kama ndege aliyepotea mbali na chicha yake.


Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.


Mashamba ya Hesiboni yamefifia, vilevile na zabibu za Sibuma ambazo ziliwalewesha wakubwa wa mataifa. Zikafika Yaweri na kusambaa hata katika jangwa, chipukizi zake zikafika hata ngambo ya bahari.


Mutumwa hahesabiwi kuwa mumoja wa jamaa siku zote, lakini mwana anahesabiwa kuwa mumoja wa jamaa siku zote.


Asubui mapema Yoshua pamoja na watu wote wa Israeli walianza safari kutoka Sitimu. Walipofika kwa muto Yordani, walipiga kambi hapo kwa muda mbele ya kuvuka.


Samweli alisikia kwamba Saulo alikuwa amekwenda kule Karmeli na amesimamisha munara wa ukumbusho wake, na kwamba amekwenda Gilgali. Hivyo, kesho yake, Samweli aliamuka asubui mapema, akaenda kukutana na Saulo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ