Mungu akamujibu: “Hapana. Muke wako Sara atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita Isaka. Nitaimarisha agano langu kwake na wazao wake, kuwa agano la milele.
Lakini akawapa wana wa habara zake zawadi. Na wakati alipokuwa bado muzima, akawapeleka katika inchi ya upande wa mashariki, mbali na mwana wake Isaka.
Lakini, kama zawadi ya Mungu inatokana na Sheria, basi, haiwezi kutokana tena na ahadi. Lakini kwa njia ya ahadi, Mungu ameonyesha wema wake kwa Abrahamu.
na hivyo tutapata baraka zile ambazo Mungu aliwawekea watu wake. Baraka zisizoweza kuoza wala kuchafuka wala kupunguka; nazo zinawekewa akiba kwa ajili yenu mbinguni.
Watu hawa wametoka kati yetu, lakini hawakukuwa wa kundi letu, na kwa sababu hii wametuacha. Kama wangekuwa wa kundi letu, wangekaa pamoja nasi. Lakini wametuacha kusudi ionekane wazi ya kama hawakukuwa wa kundi letu.
Gileadi alikuwa vilevile na wana wengine toka kwa muke wake. Watoto wa muke huyo walipokuwa wakubwa, wakamufukuza Yefuta kutoka kwao, wakamwambia: “Wewe hauna haki ya kupata urizi kutoka kwa baba yetu, maana wewe ni mutoto wa mwanamuke mwingine.”