Mungu akamujibu: “Hapana. Muke wako Sara atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita Isaka. Nitaimarisha agano langu kwake na wazao wake, kuwa agano la milele.
Mumoja wao akasema: “Hakika nitakurudilia kwa wakati kama huu katika mwaka na muke wako Sara atakuwa na mutoto mwanaume.” Sara alikuwa kule nyuma kwenye mulango wa hema, akisikiliza.
Kisha Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawafikia kwa kuwasaidia. Atawatoa katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”
Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.
Kwenda uwakusanye wazee wa Israeli na kuwaambia kwamba: Yawe, Mungu wa babu wao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, amekutokea na kusema: ‘Nimewachunguza ninyi na kuyaona mambo munayotendewa katika inchi ya Misri!
Kisha, Naomi akapata habari kwamba Yawe alikuwa amewabariki watu wake kwa kuwapa chakula. Basi, akaondoka kutoka Moabu kurudi kwao, pamoja na wakwe zake.
Kesho yake asubui, Elekana na jamaa yake waliamuka asubui mapema, na kisha kumwabudu Yawe, walirudi kwao Rama. Elekana akalala na muke wake Hana na Yawe akamukumbuka.