Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 20:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Sasa umurudishe yule mwanamuke kwa mume wake. Abrahamu ni nabii. Atakuombea nawe utaishi. Lakini usipomurudisha, ujue kwa hakika kwamba wewe utakufa pamoja na watu wako wote.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 20:7
42 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakubwa wa mufalme wa Misri walipomwona Sarai, wakamusifia kwa mufalme. Basi, Sarai akapelekwa ndani ya nyumba ya yule mufalme.


Lakini Yawe akamutesa na watu wote wa nyumba yake kwa mapigo makali kwa sababu ya Sarai, muke wa Abramu.


Lakini usikule matunda ya muti wa kujua mazuri na mabaya, maana siku utakapokula matunda ya muti ule, hakika utakufa.”


Hapo mbele Yawe alikuwa amewazuia wanawake wote wa nyumba ya Abimeleki kupata watoto kwa sababu ya Sara, muke wa Abrahamu.


Lakini Mungu akamufikia Abimeleki katika ndoto usiku, akamwambia: “Wewe utakufa kwa sababu ya mwanamuke uliyemutwaa, maana yuko na mume wake.”


Basi, Abimeleki akaamuka asubui mapema, akawaita watumishi wake wote na kuwaelezea mambo aliyoona katika ndoto. Nao wakaogopa sana.


“Ee bwana wetu, usikilize; wewe ni kiongozi mukubwa kati yetu. Umuzike marehemu muke wako katika kaburi lolote utakalojichagulia; hakuna yeyote kati yetu atakayekunyima kaburi lake, wala kukuzuia kumuzika marehemu muke wako.”


Daudi alipomwona yule malaika aliyekuwa anawaua watu, alimwambia, Yawe: “Mimi ndiye ninayekuwa na kosa! Mimi mwenyewe nimekosa! Hawa watu wapole hawakufanya uovu. Ninakusihi sana uniazibu mimi na jamaa ya baba yangu.”


Basi, mufalme Yeroboamu akamwambia nabii: “Tafazali, umusihi Yawe, Mungu wako, uniombee mukono wangu upate kupona.” Naye nabii akamwomba Yawe, na mukono wa mufalme ukapona, ukarudia kwa hali yake ya zamani.


Lakini Namani alikasirika sana, akaenda zake akisema: “Nilizani kwamba hakika atanifikia na kumwomba Yawe, Mungu wake, apitishe mikono yake juu ya pahali ninapogonjwa na kuniponyesha!


“Musiwaguse wachaguliwa wangu; musiwazuru manabii wangu!”


Watu wengi kati ya wale waliotoka katika kabila la Efuraimu, Manase, Isakari na Zebuluni, walikuwa wakifanya Pasaka kinyume cha maagizo. Hii ni kwa kuwa mufalme Hezekia aliwaombea akisema: “Yawe, wewe ni mwema. Umusamehe mutu yeyote


Yeye hawapendelei wakubwa, wala kuwajali watajiri kuliko wamasikini, maana wote hao ni kazi ya mikono yake.


Kwa hiyo mutwae ngombe dume saba na kondoo dume saba, muende kwa mutumishi wangu Yobu, mutoe nyama wale kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yenu. Naye mutumishi wangu Yobu atawaombea, nami nitaisikiliza maombi yake na kuacha kuwatendea kulingana na upumbafu wenu; maana hamukusema ukweli juu yangu kama mutumishi wangu Yobu alivyofanya.”


Yawe ni rafiki ya wale wanaomwabudu; yeye anawajulisha agano lake.


Basi, Yetro akamwambia Musa: “Unavyofanya si vizuri!


Haruni ataongea na Waisraeli kwa ajili yako. Yeye atakuwa musemaji wako, nawe utakuwa kama Mungu kwake.


Yawe akamwambia Musa: “Mimi ninakufanya kuwa kama mungu kwa mufalme wa Misri, naye ndugu yako Haruni atakuwa nabii wako.


Yawe akaniambia hivi: Usiwaombee watu hawa uheri.


Kisha Yawe akaniambia: Hata kama Musa na Samweli wangesimama mbele yangu na kunisihi, singewahurumia watu hawa. Uwaondoe kabisa mbele yangu. Uwaache waende!


Ikiwa wao ni manabii, na ikiwa wana ujumbe kutoka kwa Yawe, basi wamusihi Yawe wa majeshi, kusudi vyombo vilivyobaki katika nyumba ya Yawe na katika nyumba ya mufalme wa Yuda, na katika Yerusalema, visitwaliwe na kupelekwa Babeli.


Nikimwambia mutu mwovu kwamba hakika atakufa, nawe haumwonyi au kumwambia aache mwenendo wake mubaya apate kuyaokoa maisha yake, basi, mutu huyo mwovu atakufa kwa uovu wake; lakini wewe utabeba lazima ya damu yake.


Nikimwambia mutu mwovu hivi: Wewe mutu mwovu hakika utakufa; lakini wewe hausemi chochote kwa kumwonya aachane na mwenendo wake, yule mutu atakufa kwa kosa lake; lakini nitakulaumu wewe kwa kifo chake.


Halafu kisha kubadilisha nguo zake atapeleka yale majivu inje ya kambi pahali panapokuwa safi.


Hii ndio sheria juu ya ibada inayoelekea sadaka ya vyakula. Wazao wa Haruni ndio wanaokuwa na uwezo wa kumutolea Yawe sadaka hiyo juu ya mazabahu.


Halafu Simoni akawaambia Petro na Yoane: “Muniombee ninyi wenyewe kwa Bwana, kusudi lisinipate hata neno moja kati ya maneno haya muliyosema.”


Yule anayesema kwa luga ya ajabu anajenga imani yake mwenyewe, lakini yule anayetabiri anajenga imani ya kanisa zima.


Zamani Mungu alisema na babu zetu kwa njia ya manabii, mara nyingi na kwa namna nyingi.


Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, mume na muke wake wanapaswa kujikinga na uchafu, kwa sababu Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati.


Mutu akimwona ndugu yake anafanya zambi isiyoleta kifo, anapaswa kumwombea kwa Mungu, Mungu atamupa mutu yule uzima. Jambo hili linaelekea wale wanaotenda zambi isiyoleta kifo. Maana kuna zambi inayoleta kifo lakini sisemi kama ataomba juu ya hiyo.


Hivyo wakamwambia Samweli: “Tafazali, utuombee sisi watumishi wako kwa Yawe, Mungu wako, kusudi tusikufe; kwa sababu tumezidisha zambi zetu kwa uovu huo wa kujitakia mufalme.”


Tena kwa upande wangu haitatokea niache kuwaombea kwa Yawe; kufanya hivyo itakuwa kumukosea Yawe. Nitaendelea kuwafundisha njia njema na ya haki.


Kisha, Samweli akawaita Waisraeli wote wakutane kule Misipa, akawaambia: “Kule nitamwomba Yawe kwa ajili yenu.”


Basi, wakamwambia Samweli: “Usiache kumulilia Yawe, Mungu wetu, kwa ajili yetu. Endelea kumulilia atuokoe kutokana na Wafilistini.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ