Sasa umurudishe yule mwanamuke kwa mume wake. Abrahamu ni nabii. Atakuombea nawe utaishi. Lakini usipomurudisha, ujue kwa hakika kwamba wewe utakufa pamoja na watu wako wote.”
Akaota ndoto, na katika ndoto hiyo, aliona ngazi iliyosimamishwa juu ya dunia na incha yake inafika mbinguni. Wamalaika wa Mungu walikuwa wakipanda na kushuka katika ngazi hiyo.
Kisha Yosefu akaota ndoto ingine, akawaelezea wandugu zake akisema: “Musikilize, nimeota ndoto nyingine. Nimeona jua, mwezi na nyota kumi na moja vinainamia mbele yangu.”
Basi, usiku mumoja, yule mutunza vinywaji mukubwa na yule mupishi mukubwa wa mukate wa mufalme, waliota ndoto mule ndani ya gereza, kila mumoja na ndoto yake tofauti.
Wakamujibu: “Tuna huzuni kwa sababu tumeota ndoto na hakuna anayeweza kututafsiria ndoto zetu.” Yosefu akawaambia: “Kutafsiri ndoto si kazi ya Mungu? Basi, muniambie ndoto zenu.”
Alipofika, Yona aliingia katika muji. Kisha kutembea mwendo wa siku nzima, akaanza kutangaza: Kunabaki siku makumi ine tu na muji huu wa Ninawe utaangamizwa!
Naye alipokuwa angali akifikiri juu ya maneno hayo, malaika wa Bwana akamutokea katika ndoto na kumwambia hivi: “Wewe Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumwoa muchumba wako Maria, kwa maana mimba yake imetokana na uwezo wa Roho Mutakatifu.
Pilato alipokuwa amekwisha kuikaa kwa kuamua maneno, muke wake akamutumia ujumbe huu: “Usijiingize katika maneno ya mutu huyo mwenye haki, kwa sababu usiku niliteseka sana katika ndoto kwa ajili yake.”