Basi, Sarai akamwambia Abramu: “Unajua kwamba Yawe hajanijalia kupata watoto. Umutwae Hagari mujakazi wangu. Labda nitapata watoto kutoka kwake.” Abramu akakubali shauri la Sarai.
Sasa umurudishe yule mwanamuke kwa mume wake. Abrahamu ni nabii. Atakuombea nawe utaishi. Lakini usipomurudisha, ujue kwa hakika kwamba wewe utakufa pamoja na watu wako wote.”
Hivyo, wakalipeleka Sanduku hilo la Mungu kwenye muji wa Ekuroni. Lakini Sanduku hilo la Mungu lilipofika kule, watu wa muji huo walipiga kelele: “Wametuletea Sanduku la Mungu wa Israeli kwa kutuua sisi na watu wetu.”