Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 20:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kisha Abrahamu akamwomba Mungu, naye akamuponyesha Abimeleki, muke wake na wajakazi wake, hata wakaweza kupata tena watoto.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 20:17
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Yawe akamutesa na watu wote wa nyumba yake kwa mapigo makali kwa sababu ya Sarai, muke wa Abramu.


Sasa umurudishe yule mwanamuke kwa mume wake. Abrahamu ni nabii. Atakuombea nawe utaishi. Lakini usipomurudisha, ujue kwa hakika kwamba wewe utakufa pamoja na watu wako wote.”


Yawe alipoona kwamba Lea anachukiwa, akamujalia watoto; lakini Rakeli alikuwa tasa.


Haya yote yatatendeka kusudi waweze kumutolea Mungu wa mbinguni sadaka zinazomupendeza na waombee maisha yangu mimi mufalme na watoto wangu.


Kwa hiyo mutwae ngombe dume saba na kondoo dume saba, muende kwa mutumishi wangu Yobu, mutoe nyama wale kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yenu. Naye mutumishi wangu Yobu atawaombea, nami nitaisikiliza maombi yake na kuacha kuwatendea kulingana na upumbafu wenu; maana hamukusema ukweli juu yangu kama mutumishi wangu Yobu alivyofanya.”


Yawe anajiweka mbali na watu waovu, lakini yuko karibu na wenye haki kwa kuwasikiliza.


Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Yawe, Mutakatifu wa Israeli, Mungu, Muumba wa Israeli anasema hivi: Munataka kuniuliza juu ya watoto wangu, au kuniamuru juu ya kazi zangu mwenyewe?


Musa akamulilia Yawe akisema: Ninakusihi, ee Mungu, umuponye.


Basi, watu wakamwendea Musa, wakamwambia: Tumetenda zambi kwa kumunungunikia Yawe na wewe vilevile. Umwombe Yawe atuondolee nyoka hawa. Kwa hiyo, Musa akawaombea watu.


Na kitu chochote mutakachoomba, mukiamini, mutakipata.”


“Muombe, nanyi mutapewa; mutafute, nanyi mutapata; mupige hodi, nanyi mutafunguliwa mulango.


Na manabii waliosema tangia Samweli na wale waliomufuata, wote walitangaza mambo haya yanayotokea siku hizi.


Musijisumbue juu ya neno lolote, lakini katika kila neno mutoe mahitaji yenu kwa Mungu, mukimwomba, mukimusihi na kumushukuru.


Basi muitikiane zambi ninyi kwa ninyi na kuombeana kusudi mupate kuponyeshwa. Maombi ya bidii ya mwenye haki ni yenye faida kubwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ