Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 20:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Kisha, akamwambia Sara: “Mimi nimemupa ndugu yako vikoroti elfu moja vya feza kwa kuwaonyesha wote wanaokuwa pamoja nawe kwamba hauna kosa. Umehakikishwa kwamba hauna kosa.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 20:16
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Abrahamu akamwomba Mungu, naye akamuponyesha Abimeleki, muke wake na wajakazi wake, hata wakaweza kupata tena watoto.


Si ni Abrahamu mwenyewe ndiye aliyesema kwamba huyu ni dada yake? Tena hata Sara mwenyewe alisema kwamba Abrahamu ni kaka yake! Mimi nimefanya nilivyofanya kwa moyo safi na sina kosa.”


na kumwuliza mutumishi wa Abrahamu: “Ni nani yule mutu anayetembea kule katika shamba, anakuja kutupokea?” Yule mutumishi akasema: “Ni bwana wangu.” Basi, Rebeka akatwaa kitambaa chake, akajifunika uso.


Halafu Abimeleki akawaonya watu wote akisema: “Yeyote atakayemugusa mutu huyu au muke wake, atauawa.”


Anayependa mafundisho anapenda maarifa, lakini asiyependa kuonywa ni mujinga.


Onyo la mwenye hekima kwa mutu musikilivu ni bora kuliko pete au ushanga wa zahabu safi.


Afazali mutu anayekuonya waziwazi, kuliko yule anayeficha upendo.


Kapiteni wa mashua akamwendea, akamwambia: Namna gani wewe unaweza kulala? Amuka umwombe Mungu wako; labda Mungu wako atatuhurumia na kuyaokoa maisha yetu.


Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ