Wakati Mungu aliponifanya niache nyumba ya baba yangu na kwenda kutangatanga, nilimwambia muke wangu: ‘Popote tutakapokwenda, tafazali useme kwamba mimi ni kaka yako!’ ”
Watu wa kule walipomwuliza juu ya muke wake, akajibu: “Huyu ni dada yangu.” Aliogopa kusema kwamba ni muke wake kwa kuogopa kwamba wakaaji wa inchi wangemwua kwa sababu ya Rebeka, maana Rebeka alikuwa muzuri sana.
Kwa upande wangu, siwezi kuvumilia haya hiyo. Na kwa upande wako, utakuwa mumoja wa wapumbafu wa Israeli. Basi, mimi ninakusihi uzungumuze na mufalme maana hatakukataza kunioa.”