Mwanzo 2:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20029 Yawe Mungu akaotesha kutoka udongo kila aina ya miti ya kupendeza macho na inayofaa kwa chakula. Katikati ya bustani hiyo kulikuwa muti wa uzima na muti wa kujua mazuri na mabaya. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Kwa uzuri na ukubwa wa muti huo, hakuna muti wowote katika bustani ya Edeni ambao uliweza kulinganishwa nao. Sasa, muti huo ni wewe Mufalme wa Misri. Wewe utatupwa chini kwa wafu pamoja na miti ya Edeni. Utalala karibu na wale wasiomujua Mungu na wale waliouawa kwa upanga. Hiyo itakuwa hali yako ewe Mufalme wa Misri, wewe na watu wako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
Kisha kwa ukingo wa muto huo kutaota kila namna ya miti inayotoa chakula. Majani yake hayatanyauka wala miti hiyo haitaacha kuzaa matunda. Itazaa matunda mapya kila mwezi, kwa sababu inapata maji yanayotiririka kutoka hekalu la Mungu. Matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatatumika kwa kuponyesha magonjwa.