Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 2:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kisha Yawe Mungu akapanda bustani kule Edeni, upande wa mashariki, na mule akamuweka yule mwanaume aliyemwumba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 2:8
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Loti akainua macho yake, akaona bonde la muto Yordani, akaona kwamba lina maji ya kutosha kila pahali, kama vile bustani ya Yawe na kama vile inchi ya Misri upande wa Soari. (Hii ilikuwa mbele Yawe hajaiangamiza miji ya Sodoma na Gomora).


Basi, Yawe Mungu akamufukuza Adamu inje ya bustani ya Edeni, kusudi alime udongo ambamo alitwaliwa.


Alimufukuza inje. Akaweka makerubi upande wa mashariki wa bustani ya Edeni wakiwa na upanga wa moto uliogeuka huku na kule, kwa kulinda njia inayokwenda kwenye muti wa uzima.


Kisha Kaina akaondoka mbele ya Yawe, akaenda kuishi katika inchi ya Nodi, upande wa mashariki wa Edeni.


Miungu ya mataifa iliokoa Gozani, Harani, na Resefu na Waedeni waliokaa Telasari, mataifa ambayo babu zangu waliyaangamiza?


Mimi Yawe nitaufariji Sayuni, nitatengeneza pahali pake pote palipoharibika. Nitazifanya mbuga zake kama shamba la Edeni, jangwa yake kama bustani ya Yawe. Ndani yake kutapatikana furaha na shangwe, na nyimbo za shukrani zitasikilika humo.


Wakaaji wa miji ya Harani, Kane na Edeni na wachuuzi wa Asuria na Kilmadi walifanya biashara nawe.


Ulikaa Edeni, bustani ya Mungu. Ulipambwa kwa kila namna ya mawe ya bei kali, akiki, topazi, yaspi, zabarajadi, berili, sardoniki, yakuti samawi, almasi na zumaridi. Ulikuwa na mapambo ya zahabu. Yote uliwekewa tayari siku ulipoumbwa.


Niliyafanya mataifa yatetemeke kwa sauti ya kuanguka kwake, wakati nilipouangusha chini katika kuzimu pamoja na wale wanaoshuka ndani ya shimo kwa wafu. Nayo miti yote ya Edeni, miti mizuri na ya pekee ya Lebanoni ambayo ilimwangiliwa maji, ilifarijiwa huko chini kwa wafu.


Kwa uzuri na ukubwa wa muti huo, hakuna muti wowote katika bustani ya Edeni ambao uliweza kulinganishwa nao. Sasa, muti huo ni wewe Mufalme wa Misri. Wewe utatupwa chini kwa wafu pamoja na miti ya Edeni. Utalala karibu na wale wasiomujua Mungu na wale waliouawa kwa upanga. Hiyo itakuwa hali yako ewe Mufalme wa Misri, wewe na watu wako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Kama vile moto unavyoteketeza, Jeshi hilo linaharibu kila kitu mbele yake na kuacha nyuma kila kitu kinateketezwa; mbele ya kupita kwao, inchi ni kama bustani ya Edeni, lakini wakisha kupita, ni jangwa tupu. Hakuna kinachoweza kuponyoka!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ