22 Na huo ubavu Yawe Mungu alioutoa kwa yule mwanaume akaufanya kuwa mwanamuke, akamuleta kwa huyo mwanaume.
Basi, Yawe akaumba kutoka udongo kila nyama wa pori na kila ndege wa anga, halafu akamuletea yule mwanaume aone atawapa majina gani. Na majina aliyowapa viumbe hao, yakakuwa ndiyo majina yao.
Wimbo wa safari za kidini: wa Solomono. Yawe asipoijenga nyumba, wanaoijenga wanajisumbua bure. Yawe asipoulinda muji, wanaoulinda wanakesha bure.
Anayemupata muke amepata kizuri; ni zawadi kutoka kwa Yawe.
Nyumba na mali ni urizi mutu anaopata kwa babu zake, lakini muke mwenye akili anatoka kwa Yawe.
Kwa maana, Adamu ndiye aliyeumbwa wa kwanza, na kisha Eva.
Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, mume na muke wake wanapaswa kujikinga na uchafu, kwa sababu Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati.