Wazao wa Isimaeli walikaa katika eneo lililokuwa kati ya Havila na Shuri, upande wa mashariki wa Misri, kuelekea Ashuri. Walikaa kwa utengano na wazao wengine wa Abrahamu.
Nitawachochea Wababeli na Wakaldea wote, watu toka Pekodi, Soa na Koa, pamoja na Waasuria wote. Nitawachochea vijana wote wa kuvutia, maliwali, waamuzi, majemadari na waaskari wote wakiwa wapanda-farasi.
Sasa muvunje kambi yenu muendelee na safari. Muende kwenye inchi ya milima ya Waamori na maeneo ya inchi jirani katika Araba, kwenye milima na mabonde, huko Negebu na sehemu za pembeni ya bahari. Muende mpaka inchi ya Kanana, na inchi ya Lebanoni, mpaka kwenye ule muto mukubwa Furati.
Kila pahali mutakapokanyaga kwa miguu yenu patakuwa penu. Inchi yenu itaenea kutoka katika jangwa, upande wa kusini, mpaka kwenye milima ya Lebanoni upande wa kaskazini, na kutoka muto Furati upande wa mashariki, mpaka kwenye bahari ya Mediteranea upande wa magaribi.