Angalia, nina wabinti wawili ambao bado hawajalala na mwanaume. Muniruhusu niwape hao wabinti muwatendee kama vile munavyopenda. Lakini musiwatendee lolote wanaume hawa kwa sababu ni wageni wangu.”
Kama mwanaume yeyote akilala na mwanaume mwenzake sawa vile ni mwanamuke, basi, wote wawili wanapaswa kuuawa maana wamefanya jambo linalokuwa chukizo na damu yao itakuwa juu yao wenyewe.
Kutokana na mutu mumoja, yeye aliumba watu wa mataifa yote kusudi waishi katika dunia yote. Aliwapangia nyakati na kukata mipaka ya inchi wanayopaswa kukaa ndani yake.
Mukumbuke vilevile watu wa Sodoma na Gomora na wa miji iliyokuwa kandokando wanaokuwa sawasawa na wamalaika hawa. Walifanya uasherati na mambo ya kimwili yasiyokuwa ya kawaida ya asili. Watu hawa wanapokea hukumu ya moto wa milele kuwa mufano wazi kwa watu wote.