Mwanzo 19:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Loti akawasihi sana, kwa mwisho wakakubali, wakageuka na kuingia katika nyumba yake. Loti akatayarisha karamu, akachoma mikate isiyotiwa chachu, wakakula.
Akasema: “Bwana zangu, karibu katika nyumba yangu mimi mutumishi wenu. Munaweza kunawa miguu na kulala kwangu usiku wa leo. Asubui mapema mutaweza kuendelea na safari yenu.” Lakini, wao wakasema: “Hapana! Sisi tutalala huku katika barabara.”
Labani akamwambia: “Karibu kwetu wewe uliyebarikiwa na Yawe. Mbona unasimama inje? Mimi mwenyewe nimekwisha tayarisha nyumba na pahali kwa ajili ya hawa ngamia wako!”
Siku moja Elisha alikwenda Sunemu, ambako kulikuwa mama mumoja tajiri. Mama yule akamwalika Elisha kwa chakula, na toka siku hiyo ikakuwa kawaida Elisha kula chakula kwake kila mara alipopitia kule.
Yawe akaendelea kusema: “Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu. Siku ya kwanza ya siku hizo saba, mutaondoa chachu katika nyumba zenu. Mutu yeyote akikula kitu kilichotiwa chachu katika muda ule wa siku saba, anapaswa kuondolewa kati ya Waisraeli.
Kwa sababu walikuwa wameondoka Misri kwa haraka, hawakuweza kutayarisha chakula cha safari, ila tu ule unga uliopondwa bila kutiwa chachu. Basi, wakapika mikate isiyotiwa chachu.
Hakika ninawaambia kwamba hataamuka kumupatia mikate kwa sababu yeye ni rafiki yake tu, lakini sababu ya kusihi sana kwa rafiki yake, ataamuka na kumupatia vyote anavyohitaji.
Halafu bwana wake akamwambia: ‘Kwenda katika njia kwenye vijiji na pembeni ya mashamba, uwalazimishe watu wafike kuingia, kusudi nyumba yangu ipate kujaa.
Kwa hiyo tufanye karamu yetu ya Pasaka pasipo kutumia mikate iliyotiwa chachu; ni kusema pasipo zambi na uovu. Lakini tutumie mikate isiyotiwa chachu; ni kusema katika usafi na ukweli.
Maana upendo wa Kristo unatuongoza sisi tunaokubali kwamba ni mutu mumoja tu ndiye aliyekufa kwa ajili ya watu wote; maana yake wote wanashiriki katika kifo chake.
Gideoni akaenda kwake, akatayarisha mwana-mbuzi na mikate isiyotiwa chachu kutoka debe la unga. Akatia nyama ndani ya kikapu na muchuzi ndani ya chungu, kisha akamupelekea chini ya muti wa mwalo, akamupa.
Yule mwanamuke alikuwa na mwana-ngombe wake mumoja katika nyumba yake aliyenona, akamuchinja haraka, akatwaa unga wa ngano, akauponda, akatengeneza mukate usiotiwa chachu.