Mwanzo 19:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
29 Mungu alipoangamiza miji katika bonde ambamo Loti alikuwa anakaa, alimukumbuka Abrahamu kwa kumutosha Loti katika miji hiyo, kusudi Loti asiangamizwe pamoja nayo.
Kisha Mungu akamukumbuka Noa na nyama wote wa pori na wa kufugwa waliokuwa pamoja naye ndani ya chombo. Basi, Mungu akavumisha upepo juu ya inchi, maji yakaanza kupunguka.
Nikaagiza Walawi kujitakasa na kwenda kulinda milango kwa kutakasa siku ya Sabato. Ee, Mungu wangu, unikumbuke hata na kwa hili vilevile unihurumie kutokana na rehema zako kubwa.
Hata kama hao watu watatu wangalikuwa ndani ya inchi ile, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– hawangeweza kuwaokoa hata wana au wabinti zao. Wao wenyewe tu wangeokolewa, lakini inchi ile ingekuwa ukiwa.
Ewe Efuraimu, ninaweza kukuacha namna gani? Ninaweza kukutupilia, ewe Israeli namna gani? Nitaweza namna gani kukufanya kama muji wa Adama? Nitaweza namna gani kukutendea kama Zeboimu! Ninazuizwa na moyo wangu; huruma yangu imezidi kuwa motomoto.
Lakini ni kwa sababu Yawe anawapenda na anashika kiapo alichowaapia babu zenu, ndiyo maana aliwaokoa kwa nguvu zake kubwa na kuwaokoa toka katika utumwa, toka mikono ya mufalme wa Misri.
Munaweza kuirizi inchi yao si kwa sababu ninyi ni watu wa haki wenye mioyo ya usawa; lakini Yawe, Mungu wenu, anawafukuza watu hao mbele yenu kwa sababu ni waovu na anataka kuweka imara lile neno alilowaapia babu zenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo.