Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 19:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Halafu Yawe akateremusha moto mukali wa kiberiti kutoka mbinguni juu ya Sodoma na Gomora,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 19:24
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Loti akainua macho yake, akaona bonde la muto Yordani, akaona kwamba lina maji ya kutosha kila pahali, kama vile bustani ya Yawe na kama vile inchi ya Misri upande wa Soari. (Hii ilikuwa mbele Yawe hajaiangamiza miji ya Sodoma na Gomora).


Abramu akabaki katika inchi ya Kanana na Loti akakaa kati ya miji iliyokuwa katika bonde, akahamishia kambi yake Sodoma.


Basi, Yawe akawaza: “Nimufiche Abrahamu jambo ambalo nimepanga kutenda?


Jua lilikuwa limekwisha kupanda juu wakati Loti alipofika katika muji wa Soari.


Alipokuwa hajamaliza kusema, mwingine akafika, akasema: “Umeme wa radi umewachoma na kuwateketeza kondoo na watumishi. Ni mimi tu peke yangu nimepona kwa kuja kukuletea habari.”


Nyumba yake tupu, wengine wataishi ndani; kiberiti kimetawanywa katika makao yake.


Atawanyeshea waovu makaa ya moto na kiberiti; upepo mukali utakuwa ndio azabu yao.


Basi, Musa akainua fimbo yake kuelekea mbinguni. Naye Yawe akaleta mvua ya mawe na ngurumo, umeme ukapiga inchi. Yawe alinyesha mvua ya mawe juu ya inchi ya Misri,


Yawe wa majeshi asingetuachia watu wachache, tungekwisha kuwa kama watu wa Sodoma tungekuwa na hali ileile ya Gomora.


Babeli ni utukufu wa falme zote na sifa na majivuno ya Wakaldea utakuwa kama Sodoma na Gomora, wakati Mungu alipoiangamiza.


Kweli, pahali pa kumuteketeza mufalme wa Asuria pamekwisha kutayarishwa muda murefu uliopita. Pahali penyewe ni shimo kubwa na pana. Kuna moto na kuni kwa uwingi. Yawe ataupulizia pumzi yake kama kijito cha kiberiti na kuuwasha.


Mutu huyo akuwe kama miji Yawe aliyoiangusha bila huruma. Mutu huyo asikie kilio asubui, na muchana asikie kelele za vita,


Lakini kati ya manabii wa Yerusalema, nimeona mambo ya kutisha zaidi: wao wanafanya uzinzi na kusema uongo; wanawaunga mukono wanaotenda maovu hata kusikuwe mutu anayeachana na uovu. Kwangu wote wamekuwa kama watu wa Sodoma; wakaaji wake wamekuwa kama watu wa Gomora.


Kama vile Sodoma na Gomora na miji jirani yake ilivyoangamizwa, hakutakuwa mutu yeyote atakayeishi Edomu wala kufanya mashauri humo. –Ni Yawe anayesema.–


Kama vile mimi Yawe nilivyoiangamiza miji ya Sodoma na Gomora na miji ya jirani, vilevile hakutakuwa mutu yeyote atakayeishi humo. Kweli, hakuna mutu yeyote atakeyekaa huko. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kosa la watu wangu lilikuwa kubwa kuliko zambi za watu wa Sodoma, muji ambao uliteketezwa kwa rafla bila kuwa na muda wa kunyoosha mukono.


Ewe Efuraimu, ninaweza kukuacha namna gani? Ninaweza kukutupilia, ewe Israeli namna gani? Nitaweza namna gani kukufanya kama muji wa Adama? Nitaweza namna gani kukutendea kama Zeboimu! Ninazuizwa na moyo wangu; huruma yangu imezidi kuwa motomoto.


Niliwaangusha wamoja kati yenu kwa maangamizi kama nilivyoangamiza Sodoma na Gomora. Wale waliobaki kati yenu, walikuwa kama kijiti kilichookolewa katika moto. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Kwa hiyo, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli– inchi ya Moabu itakuwa kama Sodoma na ya Amoni itakuwa kama Gomora. Inchi zake zitakuwa shamba la miiba na mashimo ya chumvi, zitakuwa ukiwa milele. Watu wangu watakaobaki wataziteka, watu wa taifa langu waliobaki watazirizi.


Ninawaambia hakika kwamba kwa Siku ya hukumu muji ule utaazibiwa vikali zaidi kuliko muji Sodoma.”


Yawe ataifanya vumbi na muchanga kuwa mvua yenu, vumbi itawanyeshea mpaka muangamie.


Wataona kwamba imejaa kiberiti na chumvi, imechomwa na kuwa tupu, haikupandwa mbegu na haioti chochote. Ni kama vile ilivyokuwa wakati Yawe alipoangamiza Sodoma na Gomora, Adima na Seboimu, kwa hasira yake kali.


Hata mataifa yote yatasema: ‘Kwa nini Yawe ameitendea hivyo inchi hii? Hasira hii kubwa ina maana gani?’


Vilevile Mungu alihukumu muji wa Sodoma na Gomora na kuiteketeza kwa moto. Kwa njia hiyo, alionyesha mufano wa mambo yatakayotokea kwa watu waovu.


Mukumbuke vilevile watu wa Sodoma na Gomora na wa miji iliyokuwa kandokando wanaokuwa sawasawa na wamalaika hawa. Walifanya uasherati na mambo ya kimwili yasiyokuwa ya kawaida ya asili. Watu hawa wanapokea hukumu ya moto wa milele kuwa mufano wazi kwa watu wote.


naye vilevile atakunywa divai kali ya hasira ya Mungu iliyotengenezwa pasipo kuchangwa na maji na kumimiwa ndani ya kikombe chenye kujaa kasirani yake! Na watu kama wale, watateswa ndani ya moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto mbele ya wamalaika watakatifu na mbele ya Mwana- Kondoo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ