Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 19:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Akasema: “Bwana zangu, karibu katika nyumba yangu mimi mutumishi wenu. Munaweza kunawa miguu na kulala kwangu usiku wa leo. Asubui mapema mutaweza kuendelea na safari yenu.” Lakini, wao wakasema: “Hapana! Sisi tutalala huku katika barabara.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 19:2
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutaletewa maji kidogo kusudi munawe miguu na kupumzika chini ya muti.


Wale wamalaika wawili wakafika katika muji wa Sodoma magaribi. Loti alikuwa ameketi kwenye mulango wa muji wa Sodoma. Alipowaona, akasimama kwenda kuwapokea, akainama kwa heshima.


Loti akawasihi sana, kwa mwisho wakakubali, wakageuka na kuingia katika nyumba yake. Loti akatayarisha karamu, akachoma mikate isiyotiwa chachu, wakakula.


Labani akamwambia: “Karibu kwetu wewe uliyebarikiwa na Yawe. Mbona unasimama inje? Mimi mwenyewe nimekwisha tayarisha nyumba na pahali kwa ajili ya hawa ngamia wako!”


Yule musimamizi alipowakaribisha ndani ya nyumba kwa Yosefu, akawapa maji ya kunawa miguu yao, na punda wao akawakulisha.


Halafu Daudi alimwambia Uria: “Urudie kwako unawe miguu yako.” Uria alitoka kwa mufalme, na mara moja mufalme akamupelekea zawadi.


Musafiri hakulala inje ya nyumba yangu; nilimufungulia mulango mupita njia.


Usimutembelee jirani yako mara kwa mara, kusudi asichoke nawe na kukuchukia.


Nimekwisha kuvua nguo zangu, nitazivaa namna gani tena? Nimekwisha kunawa miguu yangu, niichafue namna gani tena?


Halafu akamugeukia yule mwanamuke na kumwambia Simoni: “Unamwona mwanamuke huyu? Niliingia ndani ya nyumba yako, nawe haukunipa maji ya kunawa miguu yangu, lakini mwanamuke huyu amenawa miguu yangu na machozi yake na kuipanguza na nywele zake.


Kisha akatia maji ndani ya bakuli, na kuanza kunawisha miguu ya wanafunzi wake na kuipanguza na kile kitambaa alichokifunga katika kiuno.


Kisha yeye na watu wa nyumba yake wakabatizwa. Naye akatusihi akisema: “Ikiwa munakubali kweli kwamba ninamwamini Bwana, basi mufike mupange ndani ya nyumba yangu.” Akatulazimisha tuitike.


Musisahau kuwakaribisha wageni, maana kwa kufanya hivi wamoja wamewakaribisha wamalaika pasipo kujua.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ