Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 19:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Walipowatosha inje ya muji, malaika mumoja wao akawaambia: “Mukimbie kwa ajili ya usalama wenu. Musiangalie nyuma wala kusimama popote katika bonde. Mukimbilie kwenye milima, musipate kuangamia.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 19:17
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Loti akainua macho yake, akaona bonde la muto Yordani, akaona kwamba lina maji ya kutosha kila pahali, kama vile bustani ya Yawe na kama vile inchi ya Misri upande wa Soari. (Hii ilikuwa mbele Yawe hajaiangamiza miji ya Sodoma na Gomora).


Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya kabulimbo; kwa hiyo wafalme wa Sodoma na Gomora walipokuwa wakikimbia vita, wakatumbukia mule, lakini wengine wakatorokea kwenye mulima.


Kutoka pale, wale watu wakashika njia kuelekea Sodoma, lakini Yawe akabaki, akisimama pamoja na Abrahamu.


Loti akamwambia: “Hapana vile, ee bwana wangu!


Harakisha! Kimbilia kule, nami sitafanya lolote mpaka utakapofika kule.” Hivyo muji ule ukaitwa Soari.


Lakini muke wa Loti aliyekuwa nyuma ya Loti, akatazama nyuma, akageuka nguzo ya chumvi.


Loti aliogopa kuishi katika muji wa Soari, kwa hiyo akahama toka muji ule, yeye pamoja na wabinti zake wawili, wakakwenda kuishi ndani ya pango kwenye milima.


Basi, kama ukitaka kuyaokoa maisha yako na ya mwana wako Solomono, ninakushauria hivi:


Elia akakimbilia katika muji wa Beri-Seba katika jimbo la Yuda, kule alikomwacha mutumishi wake,


Wimbo wa safari za kidini. Ninainua macho kwenye milima. Musaada wangu unatoka wapi?


Mukimbie! Mujiokoe wenyewe! Mukimbie kama punda wa pori katika jangwa!


Alipofika, akawaambia watu: Tafazali muondoke kwenye hema za watu hawa waovu na musiguse kitu chao chochote, musiangamizwe pamoja nao kwa sababu ya zambi zao zote.


Yoane alipoona Wafarisayo wengi na Wasadukayo wakimufikia kwa kubatizwa, aliwaambia: “Ninyi kikundi cha nyoka! Ni nani aliyewaambia kwamba munaweza kuponyoka azabu ya Mungu inayokaribia?


Uzima unapita chakula, nao mwili ni wa lazima kuliko nguo.


Lakini Yesu akamujibu: “Mutu yeyote anayeanza kulima na kuanza tena kuangalia nyuma hafai kutumika katika Ufalme wa Mungu.”


Basi, namna gani sisi tutaponyoka azabu kama hatushuguliki na wokovu mukubwa kama huu? Ni Bwana mwenyewe aliyetangaza kwanza habari za wokovu huu, na wale waliomusikia walihakikisha kwetu kwamba ni za kweli.


Usiku ule, Saulo akatuma watu kwenye nyumba ya Daudi wamwangalie kama yuko kusudi apate kumwua asubui. Lakini Mikali muke wa Daudi akamwambia Daudi: “Kama hauopoi maisha yako usiku huu, kesho utauawa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ