Wale watu wawili wakamwambia Loti: “Uko na mutu mwingine hapa, pengine wana wako, wabinti, wachumba wa wabinti zako au watu wengine wa jamaa yako wanaoishi katika muji huu? Uwatoshe pahali hapa haraka,
Zaidi ya hayo, munafikiri nimekuja bila amri ya Yawe kwa kuishambulia na kuiangamiza inchi hii? Yawe ndiye aliyeniambia: ‘Ushambulie inchi hii na kuiangamiza!’ ”
Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.
Yawe hakuweza kuvumilia tena matendo yenu maovu na mambo ya kuchukiza muliyotenda; ndiyo maana inchi yenu imekuwa ukiwa, jangwa, laana na bila wakaaji, kama inavyokuwa mpaka leo.
Nitaharibu pahali penu pa ibada kule juu ya milima, nitabomoa mazabahu zenu za kufukizia ubani, na kutupa maiti zenu juu ya sanamu za miungu yenu. Roho yangu itawachukia kabisa.
Na pale pale malaika wa Bwana akamwazibu Herode kwa ugonjwa kwa sababu alijitukuza kwa pahali pa Mungu. Herode akakuliwa na michango ya tumbo na kisha akakufa.
“Hayo yote yatawapata ninyi na kuwaandama mpaka muangamie kwa sababu hamukutii sauti ya Yawe, Mungu wenu, juu ya kushika amri zake na masharti aliyowapa.
Ninyi hamukulipa mishahara ya watumishi waliotumika katika mashamba yenu. Musikilize mashitaki yao! Malalamiko ya wavunaji yamefika katika masikio ya Bwana Mwenye Uwezo!
Mukumbuke vilevile watu wa Sodoma na Gomora na wa miji iliyokuwa kandokando wanaokuwa sawasawa na wamalaika hawa. Walifanya uasherati na mambo ya kimwili yasiyokuwa ya kawaida ya asili. Watu hawa wanapokea hukumu ya moto wa milele kuwa mufano wazi kwa watu wote.