Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 18:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kisha akatoka haraka akakwenda kwenye kundi la ngombe, akachagua mwana-ngombe mumoja muzuri na munono, akamupatia mutumishi ambaye aliharakisha kumuchinja na kumupika.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 18:7
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Abrahamu akarudi haraka ndani ya hema akamwambia Sara: “Tayarisha haraka vipimo vitatu vya unga bora, uuponde, uchome mikate.”


Halafu Abrahamu akachukua siagi, maziwa na ile nyama uliotayarishwa, akawatayarishia wageni hao chakula; naye akasimama karibu nao walipokuwa wakikula chini ya muti.


Loti akawasihi sana, kwa mwisho wakakubali, wakageuka na kuingia katika nyumba yake. Loti akatayarisha karamu, akachoma mikate isiyotiwa chachu, wakakula.


Ole kwenu ninyi munaolalia juu ya vitanda vya pembe za tembo na kujinyoosha juu ya matandiko yao, mukikula nyama za wana-kondoo na wana-ngombe!


Alaaniwe mutu yeyote anayenidanganya, ambaye anaahidi kwa kiapo kunitolea sadaka ya nyama safi kutoka kundi lake, lakini ananitolea sadaka ya nyama mwenye kilema. Mimi ni mufalme mukubwa, na watu wa mataifa yote wananiogopa. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Kisha akawatuma watumishi wengine, akisema: ‘Mwende kuwaambia waalikwa kwamba karamu yangu iko sasa tayari. Nimechinja ngombe na nyama wenye kunona; vitu vyote viko tayari. Muwaambie wafike kwa karamu!’


Kisha, mulete yule ngombe mwenye kunona na kumuchinja; nasi tutakula na kufurahi pamoja.


Mutumishi ule akamujibu: ‘Mudogo wako amerudia salama; kwa hiyo baba yako amechinja yule ngombe mwenye kunona.’


Lakini mwana wako huyu aliyeharibu mali yako katika ukahaba alipofika, ukamuchinjia yule ngombe mwenye kunona!’


Yule mwanamuke alikuwa na mwana-ngombe wake mumoja katika nyumba yake aliyenona, akamuchinja haraka, akatwaa unga wa ngano, akauponda, akatengeneza mukate usiotiwa chachu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ