Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 18:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Kisha Abrahamu akasema: “Ee Bwana, ninakuomba usikasirike, lakini nitasema tena mara moja tu. Labda kutapatikana watu wema kumi.” Yawe akamujibu: “Kwa ajili ya hao watu wema kumi, sitaangamiza muji ule.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 18:32
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Abrahamu akaongeza kusema: “Ee Bwana, ninaomba usinikasirikie, nami nitasema tena. Labda kutapatikana watu wema makumi tatu.” Yawe akamujibu: “Sitafanya hivyo nikiwakuta hao makumi tatu.”


Abrahamu akasema: “Nimesubutu kuzungumuza na Bwana. Labda kutapatikana watu wema makumi mbili.” Yawe akamujibu: “Kwa ajili ya hao makumi mbili, sitauangamiza.”


Halafu Yuda akamukaribia Yosefu na kumwambia: “Bwana, ninakuomba uniruhusu mimi mutumishi wako, nijitetee mbele yako kwa maneno machache. Ninakusihi usinikasirikie, maana wewe ni kama mufalme wa Misri mwenyewe.


Lakini inawezekana kwamba malaika, ambaye ni mupatanishi mumoja kati ya maelfu, atakuwa karibu na mutu yule kwa kumufunulia jambo la kufanya.


Ee Bwana, wewe ni muzuri na mwenye kusamehe, mwingi wa wema kwa wote wanaokuomba.


Basi, Yawe akaacha kuwafanyia watu wake lile jambo baya alilokuwa amesema.


Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Yawe anasema hivi: Mutu akikuta kishada cha mizabibu mizuri, watu wanasema: Tusikiharibu; kina baraka. Ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.


Mukimbie huko na huko katika Yerusalema, mupeleleze na kujionea wenyewe, muchunguze katika masoko yake. Mukiona hata mutu mumoja anayefuata sheria, mutu anayetafuta ukweli, basi Yawe atausamehe Yerusalema.


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


“Muombe, nanyi mutapewa; mutafute, nanyi mutapata; mupige hodi, nanyi mutafunguliwa mulango.


Basi, Mungu ambaye kwa nguvu yake inayofanya kazi ndani yetu, anaweza kufanya mambo makubwa zaidi yanayopita yale tunayoweza kuomba au kufikiri;


Gideoni akamwambia Mungu: “Tafazali, usinikasirikie. Ninakuomba niseme mara moja tena. Ninakuomba uniruhusu nitumie ngozi hii kwa kufanya jaribio lingine. Ninakuomba juu ya ngozi kukuwe kukavu, lakini kwenye udongo kukuwe umande.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ