Alipoinua macho yake, akaona watu watatu wakisimama mbali kidogo mbele yake. Mara tu alipowaona, akakimbia kutoka kwenye mulango wa hema yake, akakwenda kuwapokea. Alipowafikia akainama kwa heshima
Labani akamwambia: “Karibu kwetu wewe uliyebarikiwa na Yawe. Mbona unasimama inje? Mimi mwenyewe nimekwisha tayarisha nyumba na pahali kwa ajili ya hawa ngamia wako!”
Basi, Yosefu akapata kukubaliwa mbele ya Potifari, hata akakuwa mutumishi wake wa pekee. Akamufanya musimamizi wa nyumba yake na mwangalizi wa mali yake yote.
Gideoni akaenda kwake, akatayarisha mwana-mbuzi na mikate isiyotiwa chachu kutoka debe la unga. Akatia nyama ndani ya kikapu na muchuzi ndani ya chungu, kisha akamupelekea chini ya muti wa mwalo, akamupa.
Malaika wa Mungu akamwambia: “Twaa nyama na mikate isiyotiwa chachu uviweke juu ya jiwe hili. Halafu tia muchuzi juu ya mikate na nyama.” Naye akafanya hivyo.