Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 18:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Sizani kama utafanya hivyo, kuwaua watu wa haki pamoja na waovu, kutendea watu wa haki sawa na waovu. Hapana, haiwezekani! Mwamuzi wa dunia yote hataacha kutenda mambo yanayokuwa sawa!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 18:25
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Labda kuna watu wa haki makumi tano katika muji. Utauangamiza muji muzima kuliko kuuacha kwa sababu ya wale wa haki makumi tano wanaokuwa mule?


Halafu miti yote katika pori itaimba kwa furaha mbele ya Yawe anayekuja kuihukumu dunia.


Basi, sasa mumwogope Yawe, mukuwe waangalifu katika kila jambo mutakalotenda kwa sababu Yawe wetu hatavumilia upotoshaji wa haki, wala upendeleo wala upokeaji wa kituliro.”


Hata hivyo, una haki kwa kutuazibu hivyo; maana wewe umekuwa mwaminifu wakati sisi tumekuwa watenda maovu.


Kwa hiyo munisikilize, enyi wenye ujuzi. Mungu hawezi kufanya uovu hata kidogo; Mungu Mwenye Uwezo hawezi kufanya kosa.


Ni ukweli mutupu: Mungu hafanyi jambo ovu. Mungu Mwenye Uwezo hapotoshi haki hata kidogo.


Sikia! Mungu hatakataa mutu mukamilifu, wala hatasaidia waovu.


Maana, unazani Mungu anapotosha sheria? Au, Mungu Mwenye Uwezo anapotosha haki?


Mbingu zinatangaza haki ya Mungu; Mungu mwenyewe ndiye mwamuzi.


Watu wa haki watafurahi wanapoona waovu wanaazibiwa; watatembea katika damu ya watu wabaya.


Mungu ni mwamuzi wa haki; kila siku analaumu maovu.


Mungu anasema: “Mimi nimeweka wakati kamili! Wakati huo nitahukumu kwa haki.


Usimame, ee mwamuzi wa watu wote; uwaazibu wenye kiburi inavyowastahili!


Mushangilie mbele ya Yawe, maana anakuja kutawala dunia. Atahukumu ulimwengu kwa haki, atatawala mataifa kama vile inavyofaa.


Basi, nikasema ndani ya moyo wangu: “Mungu atawahukumu watu wa haki hata vilevile na waovu, maana amepanga wakati kwa kila jambo na kwa kila kazi.”


Katika maisha yangu ya bure, niliona kila kitu. Mutu wa haki anakufa ingawa ni wa haki, ambapo mutu mwovu anaendelea kuishi maisha marefu ingawa ni mwovu.


Lakini, ee Yawe wa majeshi, wewe unayehukumu kwa haki, unayechunguza mioyo na akili za watu, unijalie nione jinsi utakavyowalipiza kisasi, maana ninayaweka maneno yangu kwako.


Ee Yawe, wewe ni mwenye haki, ingawa nitakushitaki. Lakini ningependa nibishane nawe juu ya mambo ya haki: Kwa nini waovu wanafanikiwa katika mambo yao? Mbona wote wanaodanganya wanastawi?


Lakini ninyi munasema: Matendo ya Yawe si sawa! Musikilize sasa, enyi Waisraeli: Ninachofanya mimi si sawa? Munachofanya ninyi ndicho kisichokuwa sawa.


Pale ndipo mutakapotambua tena tofauti inayokuwa kati ya wenye haki na waovu, kati ya mutu anayemutumikia Mungu na asiyemutumikia.


Lakini Musa na Haruni wakajitupa uso mpaka chini na kusema: Ee Yawe unayekuwa asili ya uzima wa wanadamu wote. Mutu mumoja akikukosea, utakasirikia watu wote pamoja?


Kwa maana sisi wote tunapaswa kusimama kwa kusambishwa mbele ya tribinali ya Kristo, kusudi kila mutu alipwe kufuatana na matendo yake mema au mabaya aliyofanya alipokuwa akiishi ndani ya mwili wake.


“Wakati uleule nikawapa waamuzi wenu maagizo haya: ‘Musikilize maneno ya watu wenu. Mutoe hukumu za haki katika maneno kati ya kila mumoja na ndugu yake au na wageni wanaoishi pamoja nanyi.


Musipendelee mutu yeyote katika kutoa hukumu; mutawasikiliza bila upendeleo, wakubwa kwa wadogo. Musiogopeshwe na sura ya mutu, maana ninyi mutapaswa kuhukumu kwa ajili ya Mungu. Kukikuwa maneno ambayo ni magumu sana kwenu, mutayafikisha kwangu nami nitayasikiliza.’


Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.


Lakini ninyi mumefikia kwenye mukutano wa furaha wa wazaliwa wa kwanza wa Mungu walioandikwa majina zao katika mbingu. Mumefikia vilevile karibu na Mungu, anayekuwa mwamuzi wa watu wote na kwenye nafsi kunapokuwa roho za watu wenye haki waliofanywa kuwa wakamilifu.


Mimi sijakukosea kitu na ndiyo maana unafanya kosa unaponishambulia. Yawe ambaye ndiye Mwamuzi ataamua leo hii kati ya Waisraeli na watu wa Amoni.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ