Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 18:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Basi, Abrahamu akamukaribia Yawe, akamwuliza: “Ni kweli utawaangamiza watu wa haki pamoja na waovu?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 18:23
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Labda kuna watu wa haki makumi tano katika muji. Utauangamiza muji muzima kuliko kuuacha kwa sababu ya wale wa haki makumi tano wanaokuwa mule?


Sizani kama utafanya hivyo, kuwaua watu wa haki pamoja na waovu, kutendea watu wa haki sawa na waovu. Hapana, haiwezekani! Mwamuzi wa dunia yote hataacha kutenda mambo yanayokuwa sawa!”


Abimeleki ambaye bado hakukuwa amelala na Sara, akajibu: “Bwana, utawaua watu wasiokuwa na kosa?


Daudi alipomwona yule malaika aliyekuwa anawaua watu, alimwambia, Yawe: “Mimi ndiye ninayekuwa na kosa! Mimi mwenyewe nimekosa! Hawa watu wapole hawakufanya uovu. Ninakusihi sana uniazibu mimi na jamaa ya baba yangu.”


Anayetawala ulimwengu kwa sheria zake anachukia haki? Utasubutu kumuhukumu mwenye haki na mwenye nguvu,


Maana, unazani Mungu anapotosha sheria? Au, Mungu Mwenye Uwezo anapotosha haki?


Lakini, kwangu ni vizuri kuwa karibu na Mungu. Wewe Bwana wangu Yawe ndiwe usalama wangu. Nitatangaza mambo yote uliyotenda!


Ujitenge mbali na mashitaki ya uongo wala usiwaue wasiokuwa na kosa na wenye haki, maana mimi sitamusamehe mutu mwovu.


Mwongozi wao atakuwa mumoja wao, mutawala wao atatokea katikati yao. Nitamuruhusu kuwa karibu nami; maana, ni nani anayeweza kusubutu kuhatarisha uzima wake kwa kunikaribia? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Lakini Musa na Haruni wakajitupa uso mpaka chini na kusema: Ee Yawe unayekuwa asili ya uzima wa wanadamu wote. Mutu mumoja akikukosea, utakasirikia watu wote pamoja?


Basi tumwendee Mungu kwa moyo wa uaminifu, kwa imani kamilifu, kwa moyo uliosafishwa toka zamiri mbaya na mwili uliosafishwa na maji safi.


Basi muitikiane zambi ninyi kwa ninyi na kuombeana kusudi mupate kuponyeshwa. Maombi ya bidii ya mwenye haki ni yenye faida kubwa.


Elia alikuwa mutu kama sisi. Yeye aliomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya inchi kwa muda wa miaka mitatu na nusu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ