Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 18:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Kutoka pale, wale watu wakashika njia kuelekea Sodoma, lakini Yawe akabaki, akisimama pamoja na Abrahamu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 18:22
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha wale watu wakaondoka, wakafika pahali walipoweza kuona muji wa Sodoma; naye Abrahamu akawasindikiza.


Basi, Yawe akawaza: “Nimufiche Abrahamu jambo ambalo nimepanga kutenda?


Wale wamalaika wawili wakafika katika muji wa Sodoma magaribi. Loti alikuwa ameketi kwenye mulango wa muji wa Sodoma. Alipowaona, akasimama kwenda kuwapokea, akainama kwa heshima.


Asubui mapema, Abrahamu alikwenda pahali alipokuwa akisimama mbele ya Yawe.


Mungu alisema atawaangamiza watu wake, lakini Musa, muchaguliwa wake, aliingilia kati, akazuia hasira yake isiwaangamize.


Kisha Yawe akaniambia: Hata kama Musa na Samweli wangesimama mbele yangu na kunisihi, singewahurumia watu hawa. Uwaondoe kabisa mbele yangu. Uwaache waende!


Mutu analipwa mabaya kwa mema? Lakini, wamenichimbia shimo. Kumbuka jinsi nilivyosimama mbele yako, nikasema mema kwa ajili yao, kusudi niepushe hasira yako mbali nao.


Nilitafuta kati yao mutu mumoja atengeneze ukuta na kusimama juu ya nafasi iliyobomoka mbele yangu, kusudi ailinde inchi na kunizuia nisiiharibu, lakini sikumupata hata mumoja.


Lakini Stefano akijazwa na Roho Mutakatifu, akakaza macho kuelekea mbingu akaona mwangaza wa utukufu wa Mungu naye Yesu akisimama na mamlaka karibu na Mungu.


Mbele ya yote, ninawaonya ninyi kuwaombea watu wote. Muombe Mungu awasaidie na kuwabariki, na mumushukuru kwa ajili yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ