Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 18:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Basi, Yawe akasema: “Kuna malalamiko mengi juu ya watu wa Sodoma na Gomora, na zambi yao ni kubwa sana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 18:20
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wa Sodoma walikuwa waovu na watenda zambi wakubwa mbele ya Yawe.


kwa maana kilio kilichomufikia Yawe juu ya wakaaji wa hapa ni kikubwa sana, naye ametutuma tukuje kuwaangamiza.”


Lakini mbele ya kulala usiku, wanaume wote wa muji wa Sodoma, vijana na wazee, bila kubaki hata mumoja, wakazunguka nyumba ya Loti.


Yawe akasema: “Umefanya nini? Damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika udongo.


Mungu aliangalia dunia, akaona kwamba imeharibika kabisa, kwa maana kila mutu alifuata njia yake mbaya.


Ubaguzi wao unashuhudia juu yao; wanatangaza zambi yao kama vile watu wa Sodoma, wala hawaifichi. Ole kwao watu hao, kwa sababu wamejiletea maangamizi wenyewe.


Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi ni taifa la Waisraeli, na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda. Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake, akaona mauaji; alitazamia haki, alisikia kilio!


Nao watu wanasema: Ingawa zambi zetu zinatoa ushuhuda juu yetu, utusaidie ee Yawe kwa ajili ya heshima ya jina lako. Maasi yetu ni mengi, tumetenda zambi mbele yako.


Lakini kati ya manabii wa Yerusalema, nimeona mambo ya kutisha zaidi: wao wanafanya uzinzi na kusema uongo; wanawaunga mukono wanaotenda maovu hata kusikuwe mutu anayeachana na uovu. Kwangu wote wamekuwa kama watu wa Sodoma; wakaaji wake wamekuwa kama watu wa Gomora.


Dada yako mukubwa ni Samaria, aliyekaa upande wako wa kaskazini pamoja na wabinti zake. Dada yako mudogo ni Sodoma, aliyekaa upande wako wa kusini pamoja na wabinti zake.


Simama, uende Ninawe, ule muji mukubwa, uukaripie. Maana uovu wake umenifikia.


Ninyi hamukulipa mishahara ya watumishi waliotumika katika mashamba yenu. Musikilize mashitaki yao! Malalamiko ya wavunaji yamefika katika masikio ya Bwana Mwenye Uwezo!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ