Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 18:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Nimemuchagua yeye na wazao wake. Yeye atawafundisha wazao wake kushika njia yangu kwa kutenda kwa haki na kwa kufuata sheria yangu, nami nitawatimizia ahadi zangu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 18:19
39 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka.


Anayekubariki, nitamubariki, anayekulaani, nitamulaani. Kwa njia yako, nitabariki mataifa yote ya dunia.”


Kisha Mungu akamwambia Abrahamu: “Kwa upande wako, wewe utalishika agano langu, wewe peke yako, wazao wako na vizazi vyao vyote.


Kutokana na wazao wako mataifa yote katika dunia yatabarikiwa kwa sababu wewe umeitii amri yangu.”


Basi, Yakobo akawaambia jamaa yake na wote aliokuwa nao: “Mutupilie mbali sanamu za miungu ya kigeni munazokuwa nazo, mujitakase na kubadilisha nguo zenu.


Maana nimefuata njia za Yawe, wala sikujitenga na Mungu wangu kwa ajili ya uovu.


Nikuambie nini zaidi, mimi Daudi? Maana wewe unanijua mimi mutumishi wako, ee Bwana wangu Yawe!


“Nawe Solomono mwana wangu, umujue Mungu wa baba yako, na umutumikie kwa moyo wako wote na kwa nia nzuri; yeye Yawe anachunguza mioyo na anafahamu mipango na mafikiri ya mwanadamu. Ukimutafuta yeye, utamwona; lakini ukimwacha, atakutupilia mbali milele.


Aliwaamuru watu wa Yuda wamutafute Yawe, Mungu wa babu zao, na kutii Sheria na amri.


Wewe ndiwe Yawe, Mungu uliyemuchagua Abramu. Ukamutoa toka Uri ya Wakaldea na kumupa jina la Abrahamu.


Kila mara karamu ilipomalizika, Yobu aliita wana wake kusudi awatakase. Aliamuka asubui mapema kisha karamu, akatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya kila mumoja wao maana aliwaza: “Labda wana wangu wametenda zambi na kumutukana Mungu ndani ya mioyo yao.”


Maana Yawe anashugulikia njia ya watu wa haki; lakini njia ya waovu itaangamia.


Yawe yuko katika hekalu lake takatifu; kiti cha kifalme cha Yawe kiko mbinguni. Kwa macho yake anawachungulia wanadamu, na kujua kila kitu wanachofanya.


Ujiepushe na uovu, utende mazuri; utafute amani na kuifuatilia.


Umufundishe mutoto njia anayopaswa kufuata, naye hataiacha hata katika uzee.


Wanaokuwa wazima ndio wanaokushukuru, kama na mimi ninavyofanya leo. Wababa wanajulisha watoto wao uaminifu wako.


Kisha watatwaa mawe mapya na kujenga pahali walipobomoa. Nao watapiga nyumba hiyo lipu upya.


Kati ya mataifa yote katika ulimwengu, ni ninyi tu niliowachagua. Kwa hiyo nitawaazibu ninyi, kwa sababu ya uovu wenu wote.


Na yule aliyepata furushi mbili akafaidia zingine mbili.


Mimi ni muchungaji mwema. Ninajua kondoo wangu na kondoo wangu wananijua,


Kisha Yesu akamwuliza mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?” Basi Petro akauzika kwa sababu Yesu alimwuliza mara ya tatu kama anamupenda. Kwa hiyo akamujibu: “Bwana, unajua yote; unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia: “Tunza kondoo wangu.


Lakini Paulo akamwambia yule mukubwa wa jeshi pamoja na waaskari wengine: “Watu hawa wasipobakia ndani ya chombo hamutaokolewa.”


Na ninyi wababa musiwakasirikishe watoto wenu. Lakini muwalee na kuwaonya, mukiwatolea mashauri yanayotoka kwa Bwana.


akawaambia: “Muweke ndani ya mioyo yenu maneno yote ambayo ninawapa leo. Muwaamuru watoto wenu kusudi wafuate kwa uaminifu maneno yote ya sheria hii.


Inafaa wasaidizi wa kanisa wakuwe kila mutu na muke mumoja tu, na wanapaswa kuwa watu wenye kuongoza vizuri watoto wao pamoja na jamaa zao.


Ninakumbuka vilevile imani yako isiyokuwa ya udanganyifu, imani ile tate muzaa mama yako Loisi na mama yako Euniki waliyokuwa nayo. Ninajua hakika kwamba wewe vilevile uko nayo.


Lakini musingi uliojengwa na Mungu, unasimama imara. Nayo maneno haya yamechapwa juu ya musingi ule “Bwana anajua wale wanaokuwa wake,” na haya mengine: “Kila mutu anayesema kwamba yeye ni wa Bwana anapaswa kujitenga na maovu.”


Tena, tangia utoto wako unajua Maandiko Matakatifu yanayoweza kukupatia hekima kusudi uokolewe kwa njia ya kumwamini Kristo Yesu.


Kama hamutaki kumutumikia Yawe, basi muchague leo hii ni nani mutakayemutumikia: kama ni miungu ile ambayo wazee wenu waliitumikia ngambo ya muto Furati, au miungu ya Waamori ambao sasa munaishi katika inchi yao. Lakini mimi na jamaa yangu, tutamutumikia Yawe.”


Kisha Manoa akasema: “Sasa maneno yako yatakapotimia ni mambo gani tutakayofuata kwa ajili ya huyo mutoto? Tutafanya nini kwa ajili yake?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ