Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 18:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kwa hiyo, Sara alicheka kimoyomoyo akisema: “Mimi ni muzee, na mume wangu vilevile. Basi, nikiwa muzee hivi, nitaweza kufurahi na kupata watoto?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 18:12
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hapo Abrahamu akainama uso mpaka chini, akacheka ndani ya moyo wake akiwaza: “Itawezekana kweli mutoto kuzaliwa kwa muzee wa miaka mia moja? Na namna gani, Sara ambaye umri wake ni miaka makumi tisa, ataweza kupata mutoto?”


Kwa hiyo Yawe akamwuliza Abrahamu: “Kwa nini Sara amecheka na kujiuliza kama kweli itawezekana apate mutoto akiwa muzee?


Elisha akamwambia: “Mwaka kesho, kwa wakati kama huu, utakuwa na mutoto katika mikono yako.” Mama akamujibu: “Hapana, Bwana wangu! Wewe ni mutu wa Mungu; usinidanganye mimi mutumishi wako!”


Hapo kinywa chetu kilijaa kicheko; tulishangilia kwa furaha. Nao watu wa mataifa mengine walisema: “Yawe amewatendea mambo makubwa!”


Sikiliza binti, ufikiri! Tega sikio lako: sahau sasa taifa lako na jamaa yako.


Ingawa hivi, kwa ngambo yenu vilevile, kila mume anapaswa kumupenda muke wake kama vile anavyojipenda, na kila muke anapaswa kuheshimu mume wake.


Ni vile Sara alimutii Abrahamu, akimwita “Bwana.” Ninyi ni wabinti zake kama mukifanya mema pasipo kuogopa kitisho chochote.


Asubui, yule mwanamuke akakuja mpaka kwenye mulango wa nyumba ambamo bwana wake alikuwa, akaanguka chini pale kwenye mulango na kubakia pale mpaka kulipopambazuka kabisa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ