Hapo Abrahamu akainama uso mpaka chini, akacheka ndani ya moyo wake akiwaza: “Itawezekana kweli mutoto kuzaliwa kwa muzee wa miaka mia moja? Na namna gani, Sara ambaye umri wake ni miaka makumi tisa, ataweza kupata mutoto?”
Halafu Rakeli akamwambia baba yake: “Tafazali baba, usiuzike, maana siwezi kusimama mbele yako kwa sababu niko katika siku zangu.” Basi, Labani akatafuta sanamu za miungu yake, lakini hakuzipata.
Mwanamuke yeyote anapokuwa na ugonjwa wa mwezi, atakuwa muchafu kwa muda wa siku saba. Mutu yeyote atakayemugusa mwanamuke yule atakuwa muchafu mpaka magaribi.
Hata Elizabeti wa jamaa yako, amepata mimba, naye atazaa mutoto mwanaume, ijapokuwa yeye ni muzee. Yeye aliyekuwa akiitwa tasa, sasa huu ni mwezi wa sita wa mimba yake.
Wakati huu, Yoshua alikuwa muzee wa miaka mingi. Basi, Yawe akamwambia: “Wewe sasa umekuwa muzee wa miaka mingi, na kumebaki bado sehemu kubwa za inchi ambazo hazijatwaliwa.