Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 17:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Tangu sasa, hautaitwa tena Abramu, lakini utaitwa Abrahamu, maana nimekufanya kuwa baba ya mataifa mengi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 17:5
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Mungu akamwambia Abrahamu: “Kuelekea muke wako, hautamwita tena jina lake Sarai, lakini jina lake litakuwa Sara.


Naye akamwuliza: “Jina lako nani?” Yeye akamujibu: “Yakobo.”


Yule mutu akamwambia: “Hautaitwa Yakobo tena, lakini Israeli, kwa sababu umeshindana na Mungu na wanadamu, ukashinda.”


Mungu akamwambia: “Jina lako ni Yakobo, lakini hautaitwa hivyo tena, lakini sasa jina lako litakuwa Israeli.” Kwa hiyo Yakobo akaitwa Israeli.


naye akamutuma nabii Natani kwa Daudi kwamba amwite mutoto yule Yedidia, ni kusema “Anayependwa na Yawe”, kwa ajili ya Yawe.


Wewe ndiwe Yawe, Mungu uliyemuchagua Abramu. Ukamutoa toka Uri ya Wakaldea na kumupa jina la Abrahamu.


Wale niliowachagua nitawapa jina jipya. Lakini ninyi jina lenu watalitumia kwa kulaani; watasema: Bwana wetu Yawe awaue.


Kesho yake asubui, Pashuri akamufungua Yeremia toka minyororo ile. Yeremia akamwambia hivi: Yawe hakuiti tena jina lako “Pashuri”, lakini “Kitisho Kila Pahali”.


Katika siku za utawala wake, inchi ya Yuda itaokolewa na inchi ya Israeli itakuwa katika usalama. Naye ataitwa kwa jina la Yawe Ni Haki Yetu.


Haya ndiyo majina ya watu ambao Musa aliwatuma kwenda kupeleleza inchi ya Kanana. Musa akamupa Hosea mwana wa Nuni jina jipya, akamwita Yoshua.


Kisha akamupeleka Simoni kwa Yesu. Yesu akamwangalia, akasema: “Wewe ndiwe Simoni mwana wa Yoane, sasa utaitwa Kefa.” (Jina “Kefa” ni sawasawa na “Petro” na maana yake ni “Jiwe.”)


Ni sawa vile inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Nimekuweka kuwa babu wa mataifa mengi.” Abrahamu alimwamini Mungu, kwa hiyo yeye ni baba yetu mbele yake. Ni yeye Mungu anayewafufua wafu na kuamuru vitu visivyokuwa vipate kuwa.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda, nitamupa ile mana iliyofichwa. Na nitamupa vilevile jiwe dogo jeupe, na juu yake kumeandikwa jina jipya ambalo hakuna mutu yeyote anayelijua, isipokuwa tu yule anayelipewa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ