Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 17:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Lakini agano langu litasimama kwa Isaka ambaye Sara atakuzalia katika mwaka kwa wakati kama huu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 17:21
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akamujibu: “Hapana. Muke wako Sara atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita Isaka. Nitaimarisha agano langu kwake na wazao wake, kuwa agano la milele.


Mumoja wao akasema: “Hakika nitakurudilia kwa wakati kama huu katika mwaka na muke wako Sara atakuwa na mutoto mwanaume.” Sara alikuwa kule nyuma kwenye mulango wa hema, akisikiliza.


Kuna jambo lolote lisilowezekana kwa Yawe? Nitakurudilia wakati uliopangwa, kwa wakati kama huu katika mwaka, na Sara atakuwa na mutoto mwanaume.”


Yawe akamukumbuka Sara, akamutendea kama alivyoahidi.


Basi, Israeli akaanza safari yake pamoja na mali yake yote. Alipofika Beri-Seba, akatoa sadaka kwa Mungu wa baba yake Isaka.


Kisha Israeli akamubariki Yosefu, akisema: “Mungu ambaye babu zangu Abrahamu na Isaka walimutii katika maisha yao, Mungu ambaye ameniongoza katika maisha yangu mpaka leo,


Heri ungenificha katika kuzimu, ungenificha mpaka kasirani yako itulie, nawe ungenipimia muda kwa kunikumbuka tena.


Mungu akasikia kilio chao, naye akakumbuka agano alilofanya na Abrahamu, Isaka, na Yakobo.


Kisha Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.” Musa akafunika uso wake kwa sababu aliogopa kumwangalia Mungu.


sawa alivyoahidi babu zetu, Abrahamu na wazao wake kwa milele.”


Aliahidi kuwasikilia babu zetu huruma; na kukumbuka agano lake takatifu,


Yesu akawajibu: “Si kazi yenu kutambua siku wala nyakati Baba yangu alizopanga kwa mamlaka yake mwenyewe.


Kwa sababu hii ndiyo ahadi ya Mungu: “Kwa wakati kama huu, nitakuja tena, na Sara atazaa mutoto mwanaume.”


Kama ninyi ni watu wa Kristo, basi, ninyi ni wazao wa Abrahamu, ninyi mutakuwa warizi sawa vile Mungu alivyoahidi.


Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ