Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 17:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Hapo Abrahamu akainama uso mpaka chini, akacheka ndani ya moyo wake akiwaza: “Itawezekana kweli mutoto kuzaliwa kwa muzee wa miaka mia moja? Na namna gani, Sara ambaye umri wake ni miaka makumi tisa, ataweza kupata mutoto?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 17:17
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Abrahamu akamwambia Mungu: “Ingekuwa heri ukubali ahadi hiyo yako imwelekee Isimaeli.”


Abramu akaanguka uso mpaka chini. Naye Mungu akamwambia:


Abrahamu na Sara walikuwa wazee sana, naye Sara hangeweza tena kuzaa.


Kwa hiyo, Sara alicheka kimoyomoyo akisema: “Mimi ni muzee, na mume wangu vilevile. Basi, nikiwa muzee hivi, nitaweza kufurahi na kupata watoto?”


Abrahamu alikuwa na umri wa miaka mia moja wakati mwana wake Isaka alipozaliwa.


Naye Sara akasema: “Mungu amenipatia kicheko; yeyote atakayesikia habari hizi, atacheka pamoja nami.”


Kisha akaongeza: “Ni nani angeweza kumwambia Abrahamu kwamba mimi Sara nitanyonyesha watoto? Tena nimemuzalia mutoto mwanaume katika uzee wake!”


Daudi akainua macho yake, akamwona yule malaika wa Yawe akisimama kati ya mbingu na dunia, naye akiinua upanga wake juu ya Yerusalema tayari kuangamiza. Halafu Daudi na wazee wote walikuwa wakivaa nguo ya gunia, wakaanguka uso mpaka chini.


Kisha Yobu akasimama, akapasua nguo yake, akanyoa nywele zake, akajitupa chini na kumwabudu Mungu,


Ulionekana kama upindi wa mvua wakati wa mvua. Ulionekana kufanana na utukufu wa Yawe. Nilipouona, nilianguka uso mpaka chini, nikasikia sauti ya mutu mwenye kusema.


Gabrieli akakuja karibu na pahali niliposimama. Mimi nikaogopa sana, hata nikaanguka uso mpaka chini. Lakini akaniambia: Wewe mutu, uelewe kwamba maono uliyoyaona yanaelekea wakati wa mwisho.


Yawe akawasha moto ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya mazabahu. Watu wote walipoona huo moto wakapiga vigelegele na kuinama uso mpaka chini.


Hapo, Musa na Haruni wakaanguka uso mpaka chini mbele yao.


Lakini Musa na Haruni wakajitupa uso mpaka chini na kusema: Ee Yawe unayekuwa asili ya uzima wa wanadamu wote. Mutu mumoja akikukosea, utakasirikia watu wote pamoja?


Wakaingia ndani ya nyumba, wakamwona mutoto pamoja na mama yake, Maria. Wakapiga magoti na kumwabudu mutoto. Kisha wakafungua mizigo yao na kumutolea zawadi ya zahabu, ubani na marasi.


Zakaria akamwuliza yule malaika: “Kitu gani kitakachonijulisha kwamba maneno hayo ni ya kweli? Mimi ni muzee, na muke wangu amekwisha kuzeeka sana.”


Baba yenu Abrahamu alishangilia akitumainia kuona siku ya kuja kwangu; na wakati alipoiona, alifurahi.”


Kisha nikalala uso mpaka chini mbele ya Yawe, kama vile mbele, kwa muda wa siku makumi ine usiku na muchana. Sikukula chakula wala kunywa maji, kwa sababu ya zambi muliyokuwa mumetenda kwa kufanya maovu mbele ya Yawe kwa kumukasirikisha.


“Kwa hiyo, nikalala uso mpaka chini mbele ya Yawe siku hizo makumi ine, usiku na muchana, kwa sababu Yawe alikuwa amesema atawaangamiza.


Naye akamujibu: “Wala wenu wala wa waadui zenu! Lakini mimi ni jemadari wa jeshi la Yawe, na sasa nimefika.” Yoshua akainama chini kwa heshima, kisha akamwuliza: “Bwana wangu, unataka mimi mutumishi wako nifanye nini?”


Yoshua akapasua nguo yake, yeye pamoja na wazee wa Israeli. Wakajitupa chini ya Sanduku la Yawe mpaka magaribi; wakajitia mavumbi juu ya vichwa vyao.


Na wale wazee makumi mbili na wane wanaokaa juu ya viti vyao vya kifalme mbele ya Mungu, wakainama uso mpaka chini wakimwabudu Mungu,


Wakati alipokuwa amekwisha kukamata kizingo, vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee makumi mbili na wane wakainama uso mpaka chini mbele ya Mwana-Kondoo. Kila mumoja wao alikuwa na kinubi na vikombe vya zahabu vilivyojaa marasi, ndiyo maombi ya watu wa Mungu.


Basi wakati Manoa na muke wake walipokuwa wanaangalia ndimi za moto zikipanda juu mbinguni kutoka kwenye mazabahu, wakamwona malaika katika ndimi hizo akipanda kwenda mbinguni. Basi Manoa na muke wake wakainama uso mpaka chini.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ