Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 17:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Nitamubariki, naye atakuzalia mutoto mwanaume. Nitamubariki Sara, naye atakuwa mama wa mataifa mengi na wafalme wa mataifa watatoka kwake.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 17:16
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akawabariki na kuwaambia: “Muzae, muongezeke, na mujaze inchi na kuitawala. Mutawale samaki wa bahari, ndege wa anga, na kila kiumbe chenye uzima kinachotembea katika dunia.”


Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka.


Halafu neno la Yawe lilimufikia kusema hivi: “Huyu hatakuwa murizi wako! Mwana wako atakayetoka katika tumbo lako ndiye atakayekuwa murizi wako.”


Kisha Mungu akamwambia Abrahamu: “Kuelekea muke wako, hautamwita tena jina lake Sarai, lakini jina lake litakuwa Sara.


Mungu akamujibu: “Hapana. Muke wako Sara atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita Isaka. Nitaimarisha agano langu kwake na wazao wake, kuwa agano la milele.


Nitakufanya ukuwe na wazao wengi sana. Toka kwako nitatokeza mataifa mengi na wafalme.


Yawe akamukumbuka Sara, akamutendea kama alivyoahidi.


Basi, wakamubariki Rebeka wakisema: “Ewe dada yetu! Ukuwe mama wa maelfu kwa maelfu; wazao wako warizi miji ya waadui zao.”


Yawe akamwambia: “Mataifa mawili yako ndani ya tumbo lako; makabila mawili yatakayozaliwa nawe, yatatengana. Moja litakuwa lenye nguvu kuliko lingine, mukubwa atamutumikia mudogo.”


Tena Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Nguvu. Ujaliwe wazao wengi na kuongezeka. Taifa na kundi la mataifa watatokea kwako na wafalme watatokea katika uzao wako.


Hawa ndio wafalme waliotawala katika inchi ya Edomu, mbele mufalme yeyote hajawatawala Waisraeli:


Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.


Kwa sababu hii ndiyo ahadi ya Mungu: “Kwa wakati kama huu, nitakuja tena, na Sara atazaa mutoto mwanaume.”


Yule mwana wa mujakazi alizaliwa sawa kawaida, lakini yule wa muke huru alizaliwa kutokana na ahadi ya Mungu.


Ni vile Sara alimutii Abrahamu, akimwita “Bwana.” Ninyi ni wabinti zake kama mukifanya mema pasipo kuogopa kitisho chochote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ