Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 17:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Mwanaume yeyote asiyetahiriwa atatengwa na watu, maana atakuwa amevunja agano langu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 17:14
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Mungu akamwambia Abrahamu: “Kuelekea muke wako, hautamwita tena jina lake Sarai, lakini jina lake litakuwa Sara.


Wakawaambia: “Hatuwezi kumwoesha dada yetu kwa mutu asiyetahiriwa. Kufanya hivyo ni haya kwetu.


Mungu anayetawala tangu milele, atanisikia na kuwafezehesha waadui yangu, maana hawapendi kubadilika, wala hawamwogopi Mungu.


Yawe akaendelea kusema: “Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu. Siku ya kwanza ya siku hizo saba, mutaondoa chachu katika nyumba zenu. Mutu yeyote akikula kitu kilichotiwa chachu katika muda ule wa siku saba, anapaswa kuondolewa kati ya Waisraeli.


Katika siku hizo saba, musikuwe na chachu yoyote katika nyumba zenu. Mutu yeyote, akuwe mugeni au mwenyeji, akikula kitu kilichotiwa chachu, ataondolewa katika kusanyiko la Waisraeli.


Yeyote atakayetengeneza mafuta kama haya, au kumupakaa mutu asiyestahili kupakwa mafuta haya, mutu huyu atatengwa mbali na watu wake.


Yeyote atakayejitengenezea ubani wa aina hiyo na kuutumia kama manukato yake pekee, atatengwa mbali na watu wake.


Watu wameichafua dunia maana wamezivunja sheria za Mungu, wamegeuka mbali na masharti yake, wamelivunja agano lake la milele.


Barabara kubwa zimebaki tupu; hakuna anayesafiri kupitia ndani yao. Mapatano yanavunjwa ovyo, washuhuda wanazarauliwa. Hakuna anayejali tena maisha ya wanadamu.


Wameurudilia uovu wa babu zao ambao walikataa kusikiliza maneno yangu; wanaiabudu miungu mingine na kuitumikia. Watu wa Israeli na watu wa Yuda wamevunja agano nililofanya na babu zao.


Agano hili halitakuwa kama lile nililofanya na babu zao nilipowatoa kwa mukono wangu kutoka Misri; agano hilo walilivunja, ingawa mimi nilikuwa Bwana wao.


Mumelichafua hekalu langu kwa kuruhusu waingie humo watu wasiotahiriwa, watu wasionitii mimi, wakati mafuta na damu vinatolewa kwa ajili yangu. Hivyo, ninyi watu wangu mumelivunja agano langu kwa machukizo yenu yote.


Watu wote watakaofanya mambo hayo ya kuchukiza wanapaswa kutengwa mbali na watu wao.


Naye atakayekula nyama hiyo anapaswa kubeba lazima ya uovu wake kwa sababu amechafua kitu kitakatifu cha Yawe. Mutu huyo atatengwa na watu wake.


Mutu yeyote asiyefunga kula siku hiyo ni lazima atengwe mbali na watu wake.


Mutu yeyote akikula mafuta ya nyama aliyetolewa kwa Yawe kwa moto, atatengwa na watu wake.


Mutu yeyote akikula damu yoyote, atatengwa na watu wake.


Lakini mutu yeyote ambaye ni safi au hayuko katika safari asipofanya sikukuu ya Pasaka, atatengwa na watu wake kwa kuwa hakunitolea sadaka kwa wakati uliopangwa. Mutu huyo atabeba lazima ya zambi yake.


Basi kila mutu anayekula mukate wa Bwana au kunywa kikombe chake bila kustahili, anafanya zambi akikosea mwili na damu ya Bwana.


Kwa maana mutu akikula mukate na kunywa kikombe pasipo kutambua maana ya mwili wa Bwana, anajiletea azabu yeye mwenyewe kwa kula na kunywa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ