Yawe akaendelea kusema: “Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu. Siku ya kwanza ya siku hizo saba, mutaondoa chachu katika nyumba zenu. Mutu yeyote akikula kitu kilichotiwa chachu katika muda ule wa siku saba, anapaswa kuondolewa kati ya Waisraeli.
Katika siku hizo saba, musikuwe na chachu yoyote katika nyumba zenu. Mutu yeyote, akuwe mugeni au mwenyeji, akikula kitu kilichotiwa chachu, ataondolewa katika kusanyiko la Waisraeli.
Barabara kubwa zimebaki tupu; hakuna anayesafiri kupitia ndani yao. Mapatano yanavunjwa ovyo, washuhuda wanazarauliwa. Hakuna anayejali tena maisha ya wanadamu.
Wameurudilia uovu wa babu zao ambao walikataa kusikiliza maneno yangu; wanaiabudu miungu mingine na kuitumikia. Watu wa Israeli na watu wa Yuda wamevunja agano nililofanya na babu zao.
Agano hili halitakuwa kama lile nililofanya na babu zao nilipowatoa kwa mukono wangu kutoka Misri; agano hilo walilivunja, ingawa mimi nilikuwa Bwana wao.
Mumelichafua hekalu langu kwa kuruhusu waingie humo watu wasiotahiriwa, watu wasionitii mimi, wakati mafuta na damu vinatolewa kwa ajili yangu. Hivyo, ninyi watu wangu mumelivunja agano langu kwa machukizo yenu yote.
Lakini mutu yeyote ambaye ni safi au hayuko katika safari asipofanya sikukuu ya Pasaka, atatengwa na watu wake kwa kuwa hakunitolea sadaka kwa wakati uliopangwa. Mutu huyo atabeba lazima ya zambi yake.