Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 17:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12-13 Kila mutoto mwanaume kati yenu anapaswa kutahiriwa kwa umri wa siku nane. Vilevile watumwa waliozaliwa katika nyumba yenu au walionunuliwa kwa feza zenu kutoka kwa wageni wasiokuwa wa uzao wenu. Hiki ni kitambulisho cha agano langu katika miili yenu, agano la milele.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 17:12
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Abrahamu akamutahiri mwana wake Isimaeli, na kuwatahiri watumwa wanaume wote waliozaliwa katika nyumba yake na walionunuliwa kwa feza zake. Aliwatahiri wote siku hiyohiyo kama vile Mungu alivyomwamuru.


Isaka alipotimiza umri wa siku nane, Abrahamu akamutahiri kama alivyoamuriwa na Mungu.


Lakini mutumwa yeyote aliyenunuliwa kwa feza, nyuma ya kumutahiri, ataruhusiwa kushiriki.


Ninyi mutakuwa watu waliotakaswa kwa ajili yangu. Kwa hiyo hamutakula nyama ya nyama aliyeuawa na nyama wa pori. Nyama hiyo mutaitupia imbwa.


Mutoto huyo atatahiriwa katika siku yake ya nane.


Ilipotimia siku nane tangu mutoto alipozaliwa, wakaenda kumutahiri, nao wakataka kumupa jina la baba yake Zakaria.


Ilipotimia siku ya kumutahiri mutoto, ndiyo siku ya nane tangu alipozaliwa, wakamupa jina lake Yesu. Jina hili ni lile malaika alilojulisha mbele mama yake hajabeba mimba.


Halafu Mungu akafanya agano na Abrahamu, na kitambulisho cha kuhakikisha kwamba limeshikwa kilikuwa kutahiriwa. Kwa hiyo Abrahamu akamutahiri mwana wake Isaka alipotimiza siku nane za kuzaliwa. Naye Isaka akamutahiri mwana wake Yakobo, na Yakobo akawatahiri wana wake kumi na wawili waliokuwa babu zetu wakubwa.


Kwa maana kuonekana kwa inje kwa Muyuda si kuwa Muyuda wa kweli, wala kutahiriwa kimwili tu si kutahiriwa kwa kweli.


Nilitahiriwa nilipokuwa na umri wa siku nane. Mimi ni Mwisraeli, wa kabila la Benjamina, Mwebrania wa asili kabisa. Kuelekea mambo ya Sheria ya Kiyuda, nilikuwa Mufarisayo,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ