14 Ndiyo maana kile kisima kinaitwa “Kisima cha yule anayeishi na anayeniona”. Kisima hiki kipo kati ya Kadesi na Beredi.
Kisha wakarudi nyuma mpaka Enimisipati ni kusema Kadesi, wakapiga inchi yote ya Waamaleki, na kuwashinda Waamori waliokaa Hasasoni-Tamari.
Hagari akamuzalia Abramu mutoto mwanaume. Abramu akamwita mutoto huyo Isimaeli.
Mungu akamufumbua Hagari macho, naye akaona kisima cha maji. Akakwenda akajaza chupa maji, akamukunywesha mutoto wake.
Kwa hiyo kisima hicho kikaitwa Beri-Seba, maana wote wawili walifanya kiapo pahali pale.
Wakati ule, Isaka alikuwa ameondoka Beri-Lahai-Roi, akakaa pande za Negebu.
Nyuma ya kifo cha Abrahamu, Mungu alimubariki mwana wake Isaka. Naye Isaka akaishi karibu na kisima cha Beri-Lahai-Roi.
Wakawaendea Musa, Haruni na Waisraeli wote pamoja kule Kadesi, katika jangwa la Parani, wakatoa habari ya mambo waliyoona na kuwaonyesha matunda ya inchi.