Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 16:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kisha huyo malaika wa Yawe akamwambia: “Wewe una mimba na utazaa mutoto mwanaume; utamwita Isimaeli, maana Yawe ameyaona mateso yako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 16:11
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akamujibu: “Hapana. Muke wako Sara atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita Isaka. Nitaimarisha agano langu kwake na wazao wake, kuwa agano la milele.


Mungu akamusikia mutoto yule akilia, na malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni, akamwambia: “Una shida gani Hagari? Usiogope. Mungu amesikia sauti ya mutoto kule anapokuwa.


Walipoikaa kwa kula wakainua macho na kuona kundi la Waisimaeli wakisafiri kutoka Gileadi kwenda Misri. Ngamia wao walikuwa wakibeba ubani, zeri na manemane.


Ni nani anayewapa vibombobombo chakula chao, vitoto vyao vinaponililia mimi Mungu, na kurukaruka huku na kule kwa njaa?


“Enyi munaomwabudu Yawe, mumusifu! Mumutukuze, enyi wazao wote wa Yakobo! Mumwogope Mungu, enyi wazao wote wa Israeli!


Kisha Yawe akamwambia: “Nimeona mateso ya watu wangu wanaokuwa katika inchi ya Misri na nimesikia kilio chao kinachosababishwa na watesaji wao. Ninajua mateso yao,


Hakika, kilio cha Waisraeli kimenifikia; nimeona jinsi Wamisri wanavyowatesa.


Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”.


Lakini yule malaika akamwambia: “Zakaria, usiogope, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Muke wako Elizabeti atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita jina lake Yoane.


Utapata mimba, utazaa mutoto mwanaume, na utamwita jina lake Yesu.


Zakaria akaomba wamuletee kibao, naye akaandika maneno haya juu yake: “Jina lake ni Yoane.” Wote wakashangaa.


Hivyo Hana akapata mimba, akazaa mutoto wa kiume. Hana akamwita mutoto huyo Samweli, maana alisema: “Nimemwomba kwa Yawe.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ