Kisha Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawafikia kwa kuwasaidia. Atawatoa katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”
Hezekia akamwuliza Isaya: “Ni kitambulisho gani ambacho kitanionyesha kwamba kweli Yawe ataniponyesha na katika siku ya tatu nitaweza kwenda kwa nyumba ya Yawe?”
Watu waliovunja agano langu na kukataa kufuata masharti ya agano walilofanya mbele yangu, nitawafanya kama yule mwana-ngombe waliyemukata sehemu mbili na kupita katikati ya vipande vile.
Watu hao ndio hao wakubwa wa inchi ya Yuda, wakubwa wa muji Yerusalema, matowashi wa mufalme, makuhani, pamoja na wanainchi wote waliopita katikati ya sehemu mbili za yule mwana-ngombe.