Wazao wako nitawafanya wakuwe wengi wasihesabike, kama vile mavumbi ya inchi. Kama vile vumbi isivyoweza kuhesabika, ndivyo wazao wako hawataweza kuhesabika!
Abramu alipopata habari kwamba mwipwa wake amekamatwa kuwa mufungwa, akatoka na watu wake mashujaa mia tatu na kumi na wanane waliozaliwa katika nyumba yake, akawafuatilia waadui mpaka Dani.
Nilinunua watumwa, wajakazi, na wengine wakazaliwa katika nyumba yangu. Nilikuwa na mali mengi, makundi ya ngombe na kondoo wengi kuliko mutu yeyote aliyenitangulia kukaa Yerusalema.
Ee Yawe, wewe ni mwenye haki, ingawa nitakushitaki. Lakini ningependa nibishane nawe juu ya mambo ya haki: Kwa nini waovu wanafanikiwa katika mambo yao? Mbona wote wanaodanganya wanastawi?