Yawe, Mungu wa mbingu, aliyenitoa katika nyumba ya baba yangu na kutoka katika inchi nilimozaliwa, na ambaye alisema nami, aliniapia kwamba atawapa wazao wangu inchi hii. Yeye atamutuma malaika wake mbele yako kusudi umuletee mwana wangu muke kutoka kule.
Kisha Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawafikia kwa kuwasaidia. Atawatoa katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”
Hivi ndivyo jamaa yangu inavyokuwa mbele ya Mungu. Maana amefanya nami agano la kudumu milele; agano kamili na lenye kuwa imara. Naye atanifanikisha katika mahitaji yangu yote.
Daudi vilevile alimushinda Hadadezeri mwana wa Rehobu, mufalme wa Zoba. Daudi alipata ushindi huu wakati Hadadezeri alipokuwa katika njia kwenda kulirudisha eneo la muto Furati kuwa chini ya utawala wake.
Solomono alitawala falme zote kuanzia kwa muto Furati mpaka katika inchi ya Wafilistini, na kuendelea hata kwa mupaka na Misri. Mataifa yote yalimutumikia na kulipa kodi kwake wakati wote wa maisha yake.
Vilevile, kwa maana makundi yao ya nyama iliongezeka kwa wingi sana, walisambaa upande wa mashariki mpaka kwenye viingilio vya jangwa lililoenea mpaka kwenye muto Furati.
Naye Solomono kwa muda wa siku saba alifanya sikukuu pamoja na kusanyiko kubwa la watu wote wa Israeli waliotoka kwenye kiingilio cha Hamati mpaka kwenye muto wa Misri.
Ukamwona kuwa wa haki mbele yako; ukafanya agano naye kuwapa wazao wake inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgasi. Na ahadi yako ukaitimiza; maana wewe ni mwaminifu.
Musa akaendelea kuwaambia watu: “Vilevile, wakati Yawe atakapowafikisha katika inchi ya Wakanana na kuwapa inchi ile kama vile alivyowaapia ninyi na babu zenu,
na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Uwakumbuke watumishi wako, Abrahamu, Isaka na Israeli, ambao uliwaapia kwa nafsi yako mwenyewe, ukisema: Nitawazidisha wazao wenu kama nyota za mbinguni na inchi yote hii niliyowaahidia nitawapa vizazi vyenu wairizi milele.
Nitafukuza mataifa mengine mbele yenu na kupanua mipaka yenu. Hakuna mutu yeyote atakayetamani inchi yenu wakati munapokusanyika kwa kuniabudu, mimi Yawe, Mungu wenu, mara tatu kila mwaka.
Hapana! Kwa ajili yao nitakumbuka agano nililofanya na wazee wao ambao niliwatoa katika inchi ya Misri, mataifa yakishuhudia, kusudi mimi nikuwe Mungu wao. Mimi ni Yawe.
Kule Mungu hakumupa Abrahamu hata sehemu ndogo ya shamba inayokuwa kama kikanyagio cha muguu kuwa urizi wake, lakini alimwahidi kwamba atamupa inchi hii kuwa urizi wake na wa wazao wake watakaoishi nyuma yake. Wakati ule, alikuwa hana mutoto.
Kila pahali mutakapokanyaga kwa miguu yenu patakuwa penu. Inchi yenu itaenea kutoka katika jangwa, upande wa kusini, mpaka kwenye milima ya Lebanoni upande wa kaskazini, na kutoka muto Furati upande wa mashariki, mpaka kwenye bahari ya Mediteranea upande wa magaribi.
“Yawe, Mungu wenu atakapopanua inchi yenu, kama vile alivyoahidi, nanyi mutasema: ‘Tutakula nyama’ kwa sababu munapenda nyama, munaweza kula nyama kiasi munachotaka.
“Tena kama vile Yawe, Mungu wenu, akipanua mipaka ya inchi yenu, kama vile alivyowaapia babu zenu, naye akiwapatia inchi yote ambayo aliahidi kuwapatia hao babu zenu
Kisha Yawe akamwambia Musa: “Hii ndiyo inchi ile niliyomwapia Abrahamu, Isaka na Yakobo kwamba nitawapa wazao wao. Nimekuonyesha uione kwa macho yako mwenyewe, lakini hautafika huko.”
“Yawe, Mungu wenu atawafikisha kwenye inchi ambayo mutakwenda kufanya makao yenu na atafukuza mataifa mengi kutoka inchi hiyo. Mutakapoingia, atafukuza mbele yenu mataifa saba makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi: Wahiti, Wagirgasi, Waamori, Wakanana, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.
ni kusema eneo linalojulikana kama la Wakanana, kuanzia kwenye kijito cha Sihori kwa mupaka wa Misri mpaka kwenye eneo la Ekuroni kule kaskazini. Maeneo yote ya watawala watano wa Wafilistini: Gaza, Asidodi, Asikeloni, Gati na Ekuroni pamoja na eneo la Awini,
Kutoka hapo ulipita karibu na Asimoni na kufuata kijito cha Misri mpaka kufikia kwenye bahari ya Mediteranea. Hapo ndipo mupaka wa kusini wa Yuda ulipopita.