Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 15:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Siku hiyo, Yawe akafanya agano na Abramu akisema: “Ninawapa wazao wako inchi hii, toka muto Nili wa Misri mpaka ule muto mukubwa wa Furati,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 15:18
58 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yawe akamutokea Abramu, akamwambia: “Nitawapa wazao wako inchi hii.” Basi, Abramu akajenga mazabahu kwa ajili ya Yawe aliyemutokea.


Inchi hii yote unayoona nitakupa wewe na wazao wako ikuwe yenu milele.


Jina la muto wa tatu ni Tigre, nao unatiririkia upande wa mashariki wa inchi ya Asuria. Jina la muto wa ine ni Furati.


Yawe, Mungu wa mbingu, aliyenitoa katika nyumba ya baba yangu na kutoka katika inchi nilimozaliwa, na ambaye alisema nami, aliniapia kwamba atawapa wazao wangu inchi hii. Yeye atamutuma malaika wake mbele yako kusudi umuletee mwana wangu muke kutoka kule.


Nitawazidisha wazao wako wakuwe kama nyota za mbinguni na kuwapa inchi hizi zote. Kutokana na wazao wako, mataifa yote katika dunia yatabarikiwa,


Akubariki wewe pamoja na wazao wako kama alivyomubariki Abrahamu, upate kurizi inchi ambamo unakaa kama mugeni, inchi ambayo Mungu alimupa Abrahamu!”


Inchi niliyowapa Abrahamu na Isaka nitakupa wewe na wazao wako.”


Kisha Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawafikia kwa kuwasaidia. Atawatoa katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”


Hivi ndivyo jamaa yangu inavyokuwa mbele ya Mungu. Maana amefanya nami agano la kudumu milele; agano kamili na lenye kuwa imara. Naye atanifanikisha katika mahitaji yangu yote.


Daudi vilevile alimushinda Hadadezeri mwana wa Rehobu, mufalme wa Zoba. Daudi alipata ushindi huu wakati Hadadezeri alipokuwa katika njia kwenda kulirudisha eneo la muto Furati kuwa chini ya utawala wake.


Solomono alitawala falme zote kuanzia kwa muto Furati mpaka katika inchi ya Wafilistini, na kuendelea hata kwa mupaka na Misri. Mataifa yote yalimutumikia na kulipa kodi kwake wakati wote wa maisha yake.


Anashika agano alilofanya na Abrahamu, na ahadi aliyomwapia Isaka.


Vilevile, kwa maana makundi yao ya nyama iliongezeka kwa wingi sana, walisambaa upande wa mashariki mpaka kwenye viingilio vya jangwa lililoenea mpaka kwenye muto Furati.


Naye Solomono kwa muda wa siku saba alifanya sikukuu pamoja na kusanyiko kubwa la watu wote wa Israeli waliotoka kwenye kiingilio cha Hamati mpaka kwenye muto wa Misri.


Watu wengine wote waliobaki kati ya Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, ni kusema wote ambao hawakukuwa Waisraeli,


Aliwatawala wafalme wote waliokuwa kuanzia muto Furati, mpaka inchi ya Wafilistini na mpaka kwenye mupaka na Misri.


Wafalme wenye nguvu wamepata kuutawala muji ule pamoja na jimbo la upande wa magaribi wa Furati wakilipisha kodi, malipo ya kuvuka mipaka na mengine.


Ukamwona kuwa wa haki mbele yako; ukafanya agano naye kuwapa wazao wake inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgasi. Na ahadi yako ukaitimiza; maana wewe ni mwaminifu.


Alisema: “Nitawapa inchi ya Kanana, nayo itakuwa mali yenu wenyewe.”


Musa akaendelea kuwaambia watu: “Vilevile, wakati Yawe atakapowafikisha katika inchi ya Wakanana na kuwapa inchi ile kama vile alivyowaapia ninyi na babu zenu,


Mungu akasikia kilio chao, naye akakumbuka agano alilofanya na Abrahamu, Isaka, na Yakobo.


Malaika wangu atakapowaongoza na kuwafikisha katika inchi ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanana, Wahivi na Wayebusi, nami nitawaangamiza wale wote.


na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.


Uwakumbuke watumishi wako, Abrahamu, Isaka na Israeli, ambao uliwaapia kwa nafsi yako mwenyewe, ukisema: Nitawazidisha wazao wenu kama nyota za mbinguni na inchi yote hii niliyowaahidia nitawapa vizazi vyenu wairizi milele.


Mushike amri ninazowapa leo. Nitawafukuza mbele yenu Waamori, Wakanana, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.


Nitafukuza mataifa mengine mbele yenu na kupanua mipaka yenu. Hakuna mutu yeyote atakayetamani inchi yenu wakati munapokusanyika kwa kuniabudu, mimi Yawe, Mungu wenu, mara tatu kila mwaka.


Tena nilifanya agano nao kwamba nitawapa inchi ya Kanana ambako waliishi kama wageni.


Nami nitawapeleka katika inchi ile niliyoapa kumupa Abrahamu, Isaka, na Yakobo. Nitawapa inchi hiyo ikuwe yenu. Mimi ni Yawe.’ ”


Siku hiyo, Yawe atapepeta ngano yake kutokea kwenye muto Furati mpaka kwenye mupaka wa Misri, nanyi Waisraeli mutakusanywa mumojamumoja.


Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.


Uliwapa inchi hii ambayo uliahidi kuwapa babu zao, inchi inayotiririka maziwa na asali.


Nitafanya nao agano la milele, kwamba sitaacha kuwatendea mema hata kidogo; nitaweka ndani ya mioyo yao utii kwa ajili yangu kusudi wasiniache tena.


basi, hapo nami nitakumbuka agano langu na Abrahamu, Isaka na Yakobo na kukumbuka ile inchi niliyowaahidia.


Hapana! Kwa ajili yao nitakumbuka agano nililofanya na wazee wao ambao niliwatoa katika inchi ya Misri, mataifa yakishuhudia, kusudi mimi nikuwe Mungu wao. Mimi ni Yawe.


Kutoka Azimoni utapinda kuelekea kijito cha Misri kwenye mupaka wa Misri na kuishia bahari ya Mediteranea.


Kule Mungu hakumupa Abrahamu hata sehemu ndogo ya shamba inayokuwa kama kikanyagio cha muguu kuwa urizi wake, lakini alimwahidi kwamba atamupa inchi hii kuwa urizi wake na wa wazao wake watakaoishi nyuma yake. Wakati ule, alikuwa hana mutoto.


Kila pahali mutakapokanyaga kwa miguu yenu patakuwa penu. Inchi yenu itaenea kutoka katika jangwa, upande wa kusini, mpaka kwenye milima ya Lebanoni upande wa kaskazini, na kutoka muto Furati upande wa mashariki, mpaka kwenye bahari ya Mediteranea upande wa magaribi.


“Yawe, Mungu wenu atakapopanua inchi yenu, kama vile alivyoahidi, nanyi mutasema: ‘Tutakula nyama’ kwa sababu munapenda nyama, munaweza kula nyama kiasi munachotaka.


“Tena kama vile Yawe, Mungu wenu, akipanua mipaka ya inchi yenu, kama vile alivyowaapia babu zenu, naye akiwapatia inchi yote ambayo aliahidi kuwapatia hao babu zenu


Kisha Yawe akamwambia Musa: “Hii ndiyo inchi ile niliyomwapia Abrahamu, Isaka na Yakobo kwamba nitawapa wazao wao. Nimekuonyesha uione kwa macho yako mwenyewe, lakini hautafika huko.”


“Yawe, Mungu wenu atawafikisha kwenye inchi ambayo mutakwenda kufanya makao yenu na atafukuza mataifa mengi kutoka inchi hiyo. Mutakapoingia, atafukuza mbele yenu mataifa saba makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi: Wahiti, Wagirgasi, Waamori, Wakanana, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.


Mungu wa amani, aliyemufufua Bwana wetu Yesu ambaye ni Muchungaji mukubwa wa kondoo kwa njia ya kumwanga damu yake inayohakikisha agano la milele,


ni kusema eneo linalojulikana kama la Wakanana, kuanzia kwenye kijito cha Sihori kwa mupaka wa Misri mpaka kwenye eneo la Ekuroni kule kaskazini. Maeneo yote ya watawala watano wa Wafilistini: Gaza, Asidodi, Asikeloni, Gati na Ekuroni pamoja na eneo la Awini,


Kutoka hapo ulipita karibu na Asimoni na kufuata kijito cha Misri mpaka kufikia kwenye bahari ya Mediteranea. Hapo ndipo mupaka wa kusini wa Yuda ulipopita.


Sauti ile ikamwambia yule malaika wa sita aliyeshika baragumu hivi: “Uwafungue wale wamalaika wane waliofungwa kwenye muto mukubwa Furati.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ