Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 15:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Hata hivyo, nitaazibu taifa watakalotumikia na kwa mwisho watatoka wakiwa na mali nyingi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 15:14
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Israeli akamwambia Yosefu: “Kama vile unavyoona, mimi niko karibu kufa. Hata hivyo, Mungu atakuwa pamoja nanyi, na kuwarudisha katika inchi ya babu zenu.


Kisha Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawafikia kwa kuwasaidia. Atawatoa katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”


Alikumbuka ahadi yake takatifu aliyomupa Abrahamu mutumishi wake.


Yawe atawatetea watu wake; na kuwaonea huruma watumishi wake.


Alifanya miujiza na maajabu kwako, ee Misri, mufalme wa Misri na wakubwa wake wote.


Unisafishe kabisa kosa langu; unitakase zambi yangu.


Katikati ya usiku, Yawe akawaua wazaliwa wa kwanza wote wa Misri. Wote walikufa, tangu muzaliwa wa kwanza wa mufalme wa Misri, murizi wa ufalme, mpaka muzaliwa wa kwanza wa mufungwa katika kifungo. Hata wazaliwa wa kwanza wa nyama nao walikufa.


Sasa, nitakutuma kwa mufalme wa Misri kusudi uwatoe watu wangu, watu wale wa Israeli, kutoka katika inchi ya Misri.”


Lakini mimi nitaazibu taifa lile litakalowafanya kuwa watumwa. Kisha nitawaondoa katika inchi ile, nao wataniabudu kwenye nafasi hii.’


Lakini ninyi ndio watu aliowakomboa kutoka Misri katika furu la chuma. Aliwatoa huko kusudi mukuwe watu wake kama vile munavyokuwa hivi leo.


Kwa macho yetu wenyewe tulimwona akifanya vitambulisho na miujiza na mambo ya kutisha na ya ajabu juu ya Wamisri, mufalme wao na wakubwa wake.


Maana, Yawe, Mungu wetu, ndiye aliyetutoa sisi pamoja na wazee wetu katika inchi ya Misri tulikokuwa watumwa, tukayaona kwa macho yetu wenyewe matendo ya ajabu aliyotenda. Akatulinda katika safari zetu zote na kati ya watu wote ambao tulipita kati yao.


“Yakobo na jamaa yake walipokwenda Misri, na Wamisri walipowagandamiza, babu zenu walimulilia Yawe. Naye akawatuma Musa na Haruni ambao waliwatoa babu zenu katika inchi ya Misri na kuwafanya mukae katika inchi hii.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ