Mwanzo 15:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
13 Yawe akamwambia Abramu: “Ujue hakika kwamba wazao wako watakaa kama wageni katika inchi isiyokuwa yao, watakuwa watumwa na watateswa kwa muda wa miaka mia ine.
Kisha wakamwambia mufalme: “Sisi watumishi wako tumekuja kukaa kama wageni katika inchi kwa sababu njaa ni kali kule Kanana na hakuna tena malisho kwa nyama wetu. Hivyo, bwana, tunakuomba, sisi watumishi wako, uturuhusu kukaa katika eneo la Goseni.”
Basi, Wamisri wakachagua wakubwa wawasimamie Waisraeli na kuwatesa kwa kazi ngumu. Waisraeli wakafanya kazi ya kumujengea mufalme wa Misri miji ya kuwekea akiba, Pitomu na Ramesesi.
Wakayafanya maisha yao kuwa magumu kwa kazi ngumu ya kutengeneza chokaa na kufyatua matofali, na kazi zote za shamba. Katika kazi zile zote, Waisraeli walitumikishwa kwa kinguvu.
Ninaahidi kwamba nitawatoa katika mateso yenu kule Misri na kuwapeleka katika inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi. Nitawapeleka katika inchi inayotiririka maziwa na asali.’
na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Huyo mugeni anayekaa nawe atakuwa kwako kama vile mwenyeji nawe utamupenda kama vile unavyojipenda mwenyewe, kwa sababu nawe ulikuwa mugeni katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
Mambo ninayotaka kusema ni haya: Mungu amekwisha kufanya agano kwa njia ya haki. Nayo Sheria iliyotokea miaka mia ine makumi tatu nyuma yake haiwezi kulivunja au kugeuza ile ahadi ya Mungu.
Usisahau kwamba wewe ulikuwa mutumwa katika inchi ya Misri, nami Yawe, Mungu wako, nikakutoa huko kwa mukono wenye nguvu na mukono ulionyooshwa. Ndiyo maana mimi Yawe, Mungu wako, nimekuamuru kushika siku ya Sabato.