Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 14:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kisha wakarudi nyuma mpaka Enimisipati ni kusema Kadesi, wakapiga inchi yote ya Waamaleki, na kuwashinda Waamori waliokaa Hasasoni-Tamari.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 14:7
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ndiyo maana kile kisima kinaitwa “Kisima cha yule anayeishi na anayeniona”. Kisima hiki kipo kati ya Kadesi na Beredi.


Abrahamu alisafiri toka kule na kuelekea eneo la Negebu, akafanya makao yake kati ya Kadesi na Suri, kisha akakwenda kukaa kwa muda kule Gerari.


Elifazi alikuwa na habara, jina lake Timuna. Huyu alimuzalia mwana, jina lake Amaleki.


Kora, Gatamu na Amaleki. Kila mumoja wao akiwa mukubwa wa kabila lake. Hao wote ni wana wa Elifazi katika inchi ya Edomu, waliotokana na Ada, muke wa Esau.


Watu wamoja wakakuja kumwambia mufalme Yosafati: “Jeshi kubwa limekuja kukushambulia kutoka Edomu, ngambo ya bahari ya Chumvi. Tayari wamekwisha kufika Hazazoni-Tamari.” (Hili ni jina lingine la Engedi).


Wavuvi watasimama kandokando ya bahari, na nafasi toka Engedi mpaka Eni-Eglaimu itakuwa ya kuanikia nyavu. Kutakuwa aina nyingi za samaki kama zinavyokuwa katika bahari ya Mediteranea.


Eneo linalopakana na kabila la Gadi kuelekea kusini, mupaka utatoka muji wa Tamari mpaka kwenye chemichemi za Meriba-Kadesi na kupitia upande wa mashariki ya Misri mpaka kwenye bahari ya Mediteranea.


Wakawaendea Musa, Haruni na Waisraeli wote pamoja kule Kadesi, katika jangwa la Parani, wakatoa habari ya mambo waliyoona na kuwaonyesha matunda ya inchi.


Mukiwashambulia Waamaleki na Wakanana, mutakufia katika vita kwa sababu mumeacha kumufuata Yawe. Yeye hatakuwa pamoja nanyi.


Halafu Waamaleki na Wakanana, waliokuwa wakiishi katika inchi hiyo ya milima, wakashuka, wakawashambulia na kuwashinda. Wakawafukuza mpaka muji wa Horma.


Waisraeli wote wakafika katika jangwa la Sinai katika mwezi wa kwanza, wakapiga kambi yao huko Kadesi. Wakiwa huko, Miriamu akakufa na kuzikwa.


Kisha Balamu akawaangalia Waamaleki, akatoa mashairi haya: Amaleki ni taifa lenye nguvu kuliko yote, lakini kwa mwisho litaangamia kabisa.


“Basi, kama vile Yawe, Mungu wetu, alivyotuamuru, tukaanza safari yetu kutoka mulima Horebu, tukapita katika lile jangwa kubwa la kutisha munalojua, kwa kufuata njia inayoelekea inchi ya milima ya Waamori. Tulipofika Kadesi-Barnea,


Basi, mukabaki kule Kadesi kwa muda murefu ambao mulikaa kule.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ