Hadadi na wenzake walisafiri kutoka Midiani, wakawakamata watu wengine kule Parani, wakaenda nao mpaka Misri, kwa mufalme wa Misri. Yeye akamupatia Hadadi nyumba, shamba, na chakula.
Wahori vilevile waliishi huko Seiri zamani, lakini wazao wa Esau wakawafukuza na kuwaangamiza, kisha wao wenyewe wakakaa katika eneo hilo pahali pao. Waisraeli wakafanya vile vile katika inchi ile ambayo Yawe aliwapa ikuwe mali yao.)
Yawe akafanya kama vile alivyowafanyia wazao wa Esau ndio Waedomu, ambao wanaishi katika inchi ya Seiri. Aliwaangamiza Wahori wakati Waedomu walipofika huko, wakanyanganya inchi yao na kuishi humo mpaka leo.